Tuesday 12 August 2014


Iringa, mkoa ambao ulishika nafasi ya tatu kitaifa katika matokeo ya mtihani wa darasa la saba mwaka 2013, yapo mambo kadhaa ya kusikitisha na ya kushangaza ambayo pengine hayapaswi kupewa nafasi katika mitihani ijayo mkoani humo.
Moja ya mambo hayo ni wanafunzi wanne katika Shule ya Msingi ya Mkombilenga iliyoko katika Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, ambao hawakufanya mtihani huo siyo kutokana na kutokuwa na sifa, bali inaelezwa kuwa waliwakimbia polisi waliokuwa wakilinda kituo hicho.
Wanafunzi hao wanne wamo katika kundi la watoro ambao ni sehemu ya wanafunzi 226 ambao hawakufanya mtihani wa kuhitimu elimu ya msingi mkoani humo mwaka jana.
Kati yao, wanafunzi 196 hawakufanya mitihani kutokana na utoro, 12 kutokana na vifo, 13 kutokana na kuwa wagonjwa na watano walipata ujauzito wakiwa shuleni.
 Lakini ukweli kuhusu polisi ni kwamba Kuwapo kwa polisi katika vituo vya mitihani ya kitaifa, hasa ya darasa la saba ni jambo ambalo limezoeleka.
Kazi ya askari hawa huwa ni kulinda usalama kwa watahiniwa na wasimamizi, lakini zaidi usalama wa mitihani yenyewe, kabla na baada ya kufanyika kwake.
Pia polisi huwa na wajibu wa kuchukua hatua dhidi ya wale ambao hubainika kufanya au kusaidia kufanyika kwa udanganyifu kwenye mitihani.
Kwa mujibu wa taratibu zilizopo, wanafunzi hupewa maelezo kuhusu mchakato wa mitihani, ambayo kufanyika kwake huwashirikisha wageni ambao ni wasimamizi kutoka nje ya shule wanazosoma wanafunzi hao na polisi ambao huwa ni walinzi wa amani.
Hata hivyo, katika baadhi ya maeneo inawezekana somo hili huwa halipewi uzito stahili au halizingatiwi ipasavyo kwa wanafunzi ambao huwa katika matarajio ya kufanya mitihani.
Kisa cha Iringa

0 comments:

Post a Comment