Friday 22 August 2014



Steve Jobs 


Yapo mambo ambayo ubongo wa binadamu unatakiwa kuyafanya kwa ufanisi ili mtu aonekane kuwa ana akili.
Mambo hayo ni kama vile kuwa na uwezo wa kujifunza na kuelewa kwa haraka, kutunza kumbukumbu na kuwa na uwezo wa kutumia tena taarifa zilizotunzwa katika ubongo ili kuzichanganua kulingana na hali halisi ya mazingira yanayomkabili.
Tunaweza kuutazama ubongo kama ilivyo kompyuta ilivyo na mfumo tata wa kuchakata taarifa ambayo utendaji wake hutegemea uwezo wa mtumiaji.
Hivyo ndivyo pia ilivyo akili ya binadamu. Akili hutegemea maumbile ya vitu vilivyomo ndani ya ubongo na mazingira ya nje,” anasema Dk Mohana Ali katika makala yake ya ‘The Biological-Environmental Hypothesis of Human Intelligence’ iliyochapishwa Julai, 2014 katika mtandao wa www.dana.org
Katika ubongo kuna nyaya zinazosafirisha taarifa kutoka seli moja kwenda seli nyingine ya ubongo. Nyaya hizi zimefunikwa na utando wa mafuta mafuta unaojulikana kama myelin.
Myelin kama ilivyo kwa vifuniko vya plastiki vinavyofunika waya wa umeme, huzuia mkondo wa taarifa katika seli za ubongo zisivuje na kwa maana hiyo huziwezesha kusafiri kwa haraka katika sehemu mbalimbali za ubongo.
Ubongo wenye myelin yenye ubora wa hali ya juu husaidia mtu kuwa na uwezo mkubwa wa kiakili.
Yapo mambo ambayo yanasaidia ubongo kuwa na afya nzuri na yanasaidia myelin kuwa katika hali nzuri. Ubongo unahitaji lishe bora na kuchangamshwa ili uweze kufanya kazi vizuri na kuwa na uwezo wa kiakili. Kwa maana hiyo akili zinalelewa na kukuzwa.
Wataalamu wa afya wanasema kuwa lishe yenye kiasi cha kutosha cha wanga na sukari ni muhimu kwa ajili ya kuupatia ubongo nguvu.
Ulaji wa samaki pia husaidia ubongo kupata mafuta mafuta ambayo ni muhimu kwa ajili ya kukuza uwezo wa kiakili.
Kucheza, kufanya mazoezi na kuvuta hewa safi ya kutosha pia ni muhimu kwa ajili ya kuchangamsha akili na kuongeza uwezo wa ubongo kufanya kazi zake kwa ufanisi.
“Akili yako inahitaji mazoezi pia. Kama utaacha kujizoeza na kutumia uwezo wa akili na ujuzi wa kutatua matatizo, uwezo wa kufikiri na utambuzi wa mambo, utategemea vipi akili yako kuwa nyingi?” anauliza mtaalamu wa tiba ya tabia katika mji wa Florida nchini Marekani, Andrea Kuszewski.

0 comments:

Post a Comment