Sunday 7 September 2014


1 (14)   
Afisa Habari, Elimu na Mawasiliano wa Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania (Law School) Bi. Scholastica Njozi akiwaeleza jambo waandishi wa habari(hawapo pichani) wakati wa ziara iliyofanywa kwenye Taasisi hiyo leo Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Afisa Habari wa Wizara ya Katiba na Sheria Bw. Omega Ngole.
5 (7) 
Mkuu wa Kitengo cha Mitihani wa Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania (Law School) Ipyana Mwaikambo akiwaeleza waandishi wa habari (Hawapo pichani), Kuhusu idadi ya wanafunzi waliodahiliwa toka Taasisi hiyo imeanzishwa ambapo alisema zaidi ya wanafunzi 4000 wameshadahiliwa mpaka sasa, wakati wa ziara iliyofanywa kwenye Taasisi hiyo leo Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Afisa Habari, Elimu na Mawasiliano wa Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania (Law School) Bi. Scholastica Njozi.
9 
Muonekano wa ndani wa Chumba cha Mahakama katika Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania (Law School)
7 (1) 

Serikali yatumia zaidi ya  Bilioni  16 kujenga Taasisi ya mafunzo ya uanasheria kwa vitendo (the law school of Tanzania).
Hayo yamesemwa  leo jijini Dar es salaam na Msemaji wa Wizara ya Katiba na Sheria Bw. Omega Ngole wakati wa ziara ya waandishi wa habari katika taasisi hiyo iliyolenga kuona hatua iliyofikiwa tangu kuanza kwa ujenzi wake mwaka 2010.
“Baada ya kukamilika kwa ujenzi huu mwaka 2013 uendeshaji wa mafunzo ulihama kutoka chuo kikuu cha Dar es salaam na kuanza kutumika kwa majengo haya ya kisasa yaliyojengwa na Serikali kupitia Wizara ya Katiba na sheria”
Akifafanua Ngole amesema ujenzi huo umehusisha ujenzi wa Mahakama ya mafunzo, (Teaching Court) vyumba vya madarasa (leacture theartres),Maktaba ya Kisasa (Library) Jengo la Utawala ( Admistration block) Mgahawa na nyumba za watumishi.
Pia Ngole alitoa wito kwa wanasheria wote wanaohitimu katika Taasisi hiyo kuwa tayari kutoa huduma popote pale nchini Tanzania kwa kuwa Serikali imetumia fedha nyingi kuanzisha Taasisi hiyo ili iwanufaishe wananchi wote.
Kwa upande wake Mkuu wa Kitengo cha mitihani  bw. Ipyana Mwaikambo alisema Taasisi hiyo imeshadahili wanafunzi zaidi ya 4000 toka kuanzishwa kwake mwaka 2008 hadi sasa.
Naye Mmoja wa wanafunzi wa Taasisi hiyo Bw. Edwin Rweykaza amesema Taasisi hiyo inatoa msisitizo katika mafunzo ya vitendo na kuwajengea uwezo wa kutimiza majukumu yao mara baada ya kuhitimu.
Kuhusu maadili Rweykaza alibainisha kuwa  ni swala linalopewa kipaumbele kwa wanafunzi wote wanaojiunga na Taasisi hiyo.
Serikali imetimiza  ndoto ya miaka mingi ya kujenga majengo ya kisasa ya Taasisi ya Mafunzo ya uanasheria kwa vitendo Tanzania (The law school of Tanzania) inayotoa mafunzo kwa vitendo kwa wahitimu wa shahada ya kwanza ya sheria wanaotarajia kufanya kazi kama mawakili kwa lengo la kuongeza stadi na ujuzi wa wanasheria hao katika kuwahudumia wananchi.

0 comments:

Post a Comment