Friday 25 July 2014

DC_adfc1.jpg
Mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya Kilolo Gerald Guninita akilakiwa na viongozi mbalimbali wa mkoa wa Iringa wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Mashujaa yaliofanyika kimkoa katika Kijiji cha Lugalo wilayani Kilolo leo. Mkuu wa wilaya huyo alimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dk. Christine Ishengoma. Kumbukumbu ya mashujaa huadhimishwa kila mwaka Julai 25, ambapo mashujaa waliopigana katika vita ya kuikomboa nchi kutoka katika utawala wa wakoloni. Sherehe za maadhimisho ya kumbukumbu ya Mashujaa zilifanyika kitaifa katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam na Mgeni Rasmi Rais Jakaya Kikwete.
NGAO_f058d.jpg
Mgeni rasmi Mkuu wa Kilolo Gerald Guninita akiweka ngao ya jadi katika mnara wa mashujaa wa jeshi la Chifu Mkwawa, mnara huo upo karibu na walipozikwa askari wa kijerumani 300 wakati wa vita vya Mkwawa mwaka 1891 wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Mashujaa yaliofanyika kimkoa katika Kijiji cha Lugalo wilayani Kilolo leo.

Mshauri wa mgambo Mkoa wa Iringa, Meja E.M. Akili akiweka  upinde kwenye mnara wa mashujaa.


RPC_145b3.jpg
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa ACP, Ramadhani Mungi akiweka silaha ya jadi (mkuki) kwenye mnara wa mfano wa mashujaa. Mnara wa mashujaa wa askari wa Chifu Mkwawa utarajia kujengwa mahali hapo karibu na mnara wa wajerumani 300 waliozikwa katika Kijiji cha Lugalo wilayani Kilolo, Mkoa wa Iringa.
MSTAAFU_fdff2.jpg
Mwanajeshi mstaafu, Magnus H. Mpinge akiweka silaha ya jadi (shoka) katika mnara.
SIME_076e2.png
Mzee wa jadi Constantino Mlawa akiweka sime kwenye mnara.
WAKAZI_230b6.jpg
Wananchi wa Kijiji cha Lugalo wilayani Kilolo, Mkoa wa Iringa akifuatilia sherehe ya maadhimisho ya siku ya mashujaa.
SOJA_3_ec0eb.jpg
Askari wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ) wakifwatua risasi za baridi hewani mara tatu kama ishara ya kuwakumbuka mashujaa wetu. (PICHA ZOTE NA FRIDAY SIMBAYA)

0 comments:

Post a Comment