Sunday 3 August 2014

Kanda ya Nyanda za Juu Kusini imetakiwa kuongeza tija katika sekta ya kilimo ili kiweze kuwa na mafanikio endelevu.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mizengo Panda alipokuwa akifungua maonesho ya Nanenane Kanda ya Nyanda za Juu Kusini baada ya kukagua mabanda hayo jijini Mbeya.

Waziri Pinda amesema kuwa katika kanda hiyo mambo mengi yameboreshwa sana katika mabanda ya maonesho ikilinganishwa na misimu iliyopita. Amesema kuwa katika kilimo cha zao la mahindi, kanda hiyo imeongeza thamani katika vifungashio. Amesema pamoja na hilo bado juhudi zinahitajika katika kuongeza tija katika uzalishaji wa mazao mengi zaidi. Amesema kuwa kilimo cha mazao ya chakula kina umuhimu mkubwa katika kanda hiyo hasa msingi wake ukijengwa katika lishe.

Aidha, Waziri Mkuu amesisitiza kilimo na ufugaji kibiashara ili kiweze kutoa mafanikio chanya. Amewataka kuwashirikisha vijana katika kilimo na ufugaji kibiashara ili mafanikio yao yaweze kuwavuta vijana wengine kushiriki katika kilimo na ufugaji.

Waziri Mkuu ameshauri kuwa viongozi wa mikoa ya Nyanda za Juu Kusini wafikirie kuipanga mikoa yao kulingana na aina kuu mazao yanayolimwa katika mikoa yao.

Waziri Pinda amepongeza kilimo cha mahindi katika ukanda huu. Amesema kuwa mahindi ni zao linalolimwa kwa asilimia 45 ya mazao yote yakilimwa na asilimia 65 ya kaya nchini. Amesema kuwa soko la zao la mahindi ni kubwa ndani na nje ya nchi. Amefarijika na kuwepo kwa baadhi ya makampuni yanayosindika zao la mahindi na kubainisha changamoto kubwa ni tija kuwa chini sana. "Afrika na Duniani Tanzania ni ya mwisho katika tija kwenye zao la mahindi" aliongea kwa uchungu Waziri Mkuu.

Warizi Mkuu amesisitiza matumizi ya mbolea katika kilimo. Amesema kuwa mbolea ni muhumu sana katika kilimo nchini na kuwataka wananchi kuachana na dhana kuwa mbolea haina muhimu katika kilimo na inaharibu udongo. Amesema kuwa umuhimu wa mbolea katika udongo unabaki palepale isipokuwa matumizi ya mbolea hutofautiana kutokana na mahitaji ya udongo.

Akiongelea matumizi ya mbegu bora, waziri mkuu amesema kuwa mbegu bora ni muhimu sana kuleta tija katika sekta ya kilimo nchini. Amesema kuwa Tanzania ina kiwango cha chini sana cha matumizi ya mbegu bora. Amesema kuwamatumizi ya mbegu bora ni asilimia 10 tu.

Maadhimisho ya 22 ya Nanenane yanaongozwa na kaulimbiu isemayo "matokeo makubwa sasa, kilimo ni biashara" yataendelea hadi kilele chake tarehe 8/8/2014.

Katika salamu za Katibu Mkuu wa TASO Nyanda za Juu Kusini, Ramadhani Kiboko amesema kuwa nyanda hiyo imejipanga kuongeza matumizi sahihi ya teknolojia. Amesema kuwa maadhimisho ya Nanenane yamekuwa yakitumika kama shamba darasa kwa watu wote kwenda kujifunza mbinu mbalimbali za kimkakati katika kuboresha kilimo nchini.

Akiongelea nafasi ya katiba mpya amesema kuwa yamewasilishwa maoni kuwa katiba mpya iondoe migogoro ya ardhi kati ya wakulima na wafugaji na kuweka uwiano wao nchini.

0 comments:

Post a Comment