Saturday 16 August 2014


Wanannchi wa mikoa ambayo haijafikiwa na awamu ya tatu ya mradi wa mfuko wa maendeleo ya jamii nchini TASAF wametakiwa wajiandae kupata maendeleo kwani mradi huo utawafikia kwa ajili ya kuzitambua kaya masikini na kiziandikisha kwa ajili ya kupeleka miradi ya maendeleo.
Akizungumza katika mahojiano maalumu na mtandao huu mkurugenzi mtendaji wa mfuko huu ndg Ladislaus Mwamanga (pichani ) amesema kwenye awamu ya tatu ya TASAF tayari mikoa ya Lindi na Mtwara imekwishafikiwa kwenye sekta ya afya, elimu na lishe bora na sasa wananchi wanafurahia maendeleo kutokana na mfuko huu kutoa fedha katika awamu nne za utekelezaji kwa miezi ya ,January, March, May na July.
Ndg Mwamanga Ameongeza kusema kuwa sasa TASAF inaendelea kuzifikia wilaya 19 za mikoa ya Dodoma, Singida na katavi kuzitambua na kuziandikisha kaya masikini.
ndg Mwamanga amesema kasi ya mafanikio inatokana na elimu wanayoitoa kwa viongozi wa halmashauri kwa ajili ya kuwaelimisha wananchi juu ya utekelezaji wa awamu ya tatu ya TASAF na hivyo kuwapongeza viongozi hao kwa ushirikiano wanaoutoa lengo likiwa ni kiwaletea maendeleo wananchi ambao ni mpango mama wa serikali.
" TASAF nado inaendelea na kasi ya kuwajengea uwezo wataalamu wa halmashauri kwa ajili ya kusambaza elimu katika wilaya nyingine hapa nchini" ambapo hadi sasa wataalamu hao wamefikia 2500 lengo likiwa ni kufikia wataalamu 4500.
Hata hivyo mkurugenzi huyo ameendelea kusema kuwa katika,mzunguko wa tatu wa TASAF halmashauri 160 zitakuwa zimekwisha fikiwa hadi kufikia mwishoni mwa mwaka huu.
Katika kipindi cha miaka kumi na mitatu ya utekelezaji wa mipango ya TASAF miradi mbalimbali ya maendeleo imewafikia wananchini kwenye sekta za afya, elimu, maji, miundombinu na barabara.
Awamu ya tatu ya utekelezaji wa mfuko wa maendeleo ya jamii nchini TASAF ilizinduliwa na rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Dk Jakaya Kikwete mwezi wa nane mwaka 2012 mjini Dodoma lengo likiwa ni kuzifikia kaya masikini nchini kwa kuzitambua na kuziandikisha kwa ajili ya kuziletea maendeleo na kuondokana na lindi la umasikini nchini.

0 comments:

Post a Comment