Friday 15 August 2014


Watoto wa shirika la kipapa (mtoto Yesu) parokia ya Mbangamao Jimbo la Mbinga mkoa wa Ruvuma, wakisherehekea siku ya maadhimisho ya miaka 50 ya uinjilishaji wa parokia hiyo. Sherehe hizo zilifanyika nje ya viwanja vya kanisa hilo.

Askofu mkuu Damian Dallu wakati akitoa mahubiri katika maadhimisho hayo kwa waumini wa kanisa Katoliki (hawapo pichani) Parokia ya Mbangamao Jimbo la Mbinga mkoani Ruvuma. (Picha zote na Julius Konala)


ASKOFU mkuu Damian Dallu, wa Jimbo kuu katoliki la Songea mkoani Ruvuma ameipongeza Parokia ya Mbangamao iliyopo katika Jimbo la Mbinga mkoani humo, kwa mchango wake mkubwa wa kusukuma maendeleo hususani katika sekta ya elimu kwa kipindi cha miaka 50 tangu kuanzishwa kwake mwaka 1964 chini ya Paroko wake wa kwanza mzalendo Hayati Askofu Maurus Komba.
Askofu Dallu ametoa pongezi hizo wakati akiwahubiria mamia ya waumini wa kanisa hilo kwenye maadhimisho ya Ibada ya misa takatifu ya shukrani, Jubilei ya miaka 50 ya parokia hiyo iliyofanyika nje ya viwanja vya kanisa hilo na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo maaskofu, mapadre, matawa, waumini pamoja na viongozi wa serikali.
Alisema Parokia hiyo kupitia Shirika la Wavisenti imefanikiwa kupanua wigo mkubwa wa kutoa huduma kwa jamii, ikiwemo kuongeza idadi ya shule za msingi hadi kufikia 15, shule za sekondari tatu na ujenzi wa shule za chekechea kwa kila kigango.
Vilevile ameeleza kuwa wameweza kutoa huduma ya maji safi na salama kwa wakazi wa eneo hilo ikiwemo pamoja na parokia hiyo kuzaa parokia mpya ya Mpepai iliyopo wilayani humo na kufanya ukarabati wa zahanati, shule za msingi na ujenzi wa sekondari. 

0 comments:

Post a Comment