Wednesday 30 July 2014

article-2710210-201DD49500000578-25_634x414

Shinji Kagawa, Darren Fletcher na Tom Cleverley, wafungaji wanne wa penati za United, wakishangilia ushindi wao wa penalti 5-3 dhidi ya Inter Milan.
article-2710210-201DD4F500000578-474_634x417
Fletcher akishangilia ushindi na kipa wa United David De Gea baada ya kushinda kwa penalti na kumpa Van Gaal rekodi ya ushindi wa asilimia 100 katika michuano hiyo.
KOCHA Louis van Gaal ameendelea kufanya vizuri kufuatia Manchester United kuitandika kwa penalti 5-3 Inter Milan baada ya sare ya 0-0 katika mechi ya Kombe la Kimataifa kujiandaa na msimu mpya nchini Marekani.

Katika mchezo huo uliofanyika kwenye Uwanja wa FedEx Field mjini Washington, penati za Man United zilizamishwa kambani na Ashley Young, Javier Hernandez, Tom Cleverley, Shinji Kagawa na Darren Fletcher wakati Marco Andreolli wa Inter aligongesha mwamba. 
ziara hiyo ya Marekana imekuwa ya mafanikio kwa Van Gaal kwani ameshinda mechi tatu mfululizo na wachezaji wake wamepata nafasi ya kumuonesha uwezo, hivyo lawama hazitegemewi.

Kocha huyo mpya wa United anaendelea kutafuta njia ya kuutekeleza mfumo wake anaoupenda wa 3-5-2.

Kwa mfano jana usiku, Man United walianza mchezo na washambuliaji wawili,  Wayne Rooney na Danny Welbeck. Walimaliza mchezo na Nani na Wilfried Zaha katika nafasi hizo.

0 comments:

Post a Comment