Wednesday 23 July 2014


Kijana anayedaiwa kuwa ni mwizi akipigwa na wananchi


 Kijana mmoja ambaye jina lake halikuweza kufahamika mara moja amepigwa na kuumizwa na wananchi wenye hasira kali katika eneo la Msasani Bonde la mpunga jijini Dares salaam baada ya kugundulika kuwa ni mwizi.
Kijana akipakizwa kwenye pikipiki tayari kabisa kuelekea kituo cha polisi jijini Dar es salaaam.

Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo wamesema kwamba kijana huyo alijaribu kuiba pikipiki iliyopaki katika eneo la macho jijini Dares salaam, baada ya kushindwa kuiwasha alitokea mmiliki na kupiga mayowe ambapo watu walifurika na kuanza kumpiga.
Mwizi huyo alikimbilia katika dispensary ya Bonde la mpunga kujificha lakini haikufua dafu kwani watu wenye hasira walizingira dispensary na kumtoa nje kwa lengo la kumpiga. Lakini baada ya muda kidogo walifika askari wa jeshi la Polisi ambapo wamemchukua na kumpeleka kituo cha polisi cha Osta bay jijini Dares saam.

Wananchi  wakimpiga kijana aliye daiwa kuwa ni mwizi.

Kijana anayedhaniwa kuwa ni mwizi,

kijana huyo akiwa na majeraha mwilini kufuatia kupigwa na wananchi.

Kijana akipelekwa katika kituo cha polisi.

Dispensari ya Bonde la mpunga sehemu aliyokimbilia kijana  huyo mwizi.

0 comments:

Post a Comment