Thursday 31 July 2014

Hatimaye Romelu Lukaku amebebwa rasmi na Everton kwa kitita cha pauni milioni 28.
Mshambuliaji huyo wa Ubelgiji mwenye miaka 21 aliyefunga mabao 16 akiwa Everton kwa mkopo msimu uliopita sasa atatumika pale Goodison Park kwa miaka mitano.
Bosi wa Everton Roberto Martinez amsemea: "Usajili huu sio tu muhimu kwa msimu huu, ni siku muhimu katika historia ya klabu."
Lukaku alijiunga Chelse akitokea Anderlecht kwa pauni milioni 18 mwezi August 2011 lakini aliichezea mechi 15 tu.
Baada ya kutia saini Lukaku amsema, "Nina miaka 21, ninahitaji kucheza kwenye Timu bora. Nataka kuwa mahali palipo nigusa kisahihi”
"Niliamua haraka sana nilitaka kurejea. Hapa ndi

chicha_0d0a3.jpg Mabingwa wa Spain, Atletico Madrid wanataka kuwasajili Santi Cazorla, 29, kutoka Arsenal, Fernando Torres, 30, kutoka Chelsea na Chicharito, 26 kutoka Manchester United (Daily Star), Chicharito amekiri kuwa hana uhakika kama ataendelea kuwepo Old Trafford akisema "Mungu pekee ndio anajua" kuhusu hatma yake (Guardian), Tottenham wanatarajia kurejea na fedha zaidi kumtaka kiungo wa Southampton Morgan Schneiderlin, licha ya Saints kusema mchezaji huyo hatoruhusiwa kuondoka (Daily Telegraph), Sporting Lisbon wamewaambia Southampton kuwa watalazimika kutoa pauni milioni 16 kumsajili beki kutoka Argentina Eric Dier, 20 (Daily Telepgraph), Marouanne Fellaini, 26 amekubali kujiunga na Napoli ya Italia, lakini Manchester United wanataka pauni milioni 18 kwa mchezaji huyo aliyenunuliwa kwa pauni milioni 27.5 mwaka jana (Daily Star), meneja wa Sunderland Gus Poyet amethibitisha kuwa wameanza tena mazungumzo ya kumsajili Fabio Borini, 23, kutoka Liverpool (Daily Express), Arsenal wanaweza kufufua mazungumzo ya kumsajili Sami Khedira, 27, kwa kuwa Real Madrid wanataka kumuuza kiungo huyo (Daily Mirror), Juventus wamekubali dau la pauni milioni 47 kutoka Manchester United kumsajili Arturo Vidal, 27, na mchezaji huyo wa Chile amekubali maslahi binafsi na Old Trafford (CaughtOffside), matumaini ya Newcastle ya kumsajili mshambuliaji Alexandre Lacazette, 23, kwa pauni milioni 10 yamegonga mwamba baada ya mchezaji huyo wa Ufaransa kusaini mkataba mpya na klabu yake (Newcastle Cronicle), Napoli wamewapa Manchester United Dries Mertens kubadilishana na Marouanne Fellaini (Daily Express), Karim Benzema amekubali kusaini mkataba mpya na Real Madrid hadi mwaka 2018 wenye thamani ya euro milioni 7 kwa mwaka (El Confidencial), Bayern Munich wameanza kumfuatilia winga wa Real Madrid Angel Di Maria ambaye anasakwa pia na Manchester United na Paris Saint-Germain (AS). Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Share na wapenda soka wote. Cheers!!(E.L)

Bi. Nasra Dafa (30) aliyeshambuliwa na mume wake wakati akiswali.
TUHUMA nzito ya aina yake ambayo haijawahi kutokea ambapo mkazi mmoja wa Tandale – Kwatumbo wilayani Kinondoni jijini DAR, Idd Mpenda anadaiwa kumshambulia na kumjeruhi hadi kuzimia mkewe, Nasra Dafa (30) wakati akiswali.Akizungumza na Amani huku akimwaga machozi, mwanamke huyo alisema tukio hilo lilijiri Julai 28, mwaka huu saa saba mchana wakati akiswali maeneo ya duka lake lililopo Tandale.
ILIKUWA KUSHTUKIZA

Alidai kwamba alikuwa katika kusujudu,  mara mumewe alitokea na kumshambulia kwa mateke, ngumi na viatu kisha akamburuza chini hadi nje hali iliyosababisha nguo aliyovaa kuvuka na kubaki kama alivyozaliwa!“ Kama unavyoniona, nimeumia sehemu mbalimbali za mwili. Kiatu ndiyo kimeniumiza sana. 

ATINGA KITUO CHA POLISI

Alisema baada ya tukio hilo kutokea  alijivuta na kuvaa gauni lingine kisha akakimbilia Kituo Kidogo cha Polisi Tandale ambapo polisi walimwambia ishu yake ni nzito na kumtaka aende Kituo cha Polisi Magomeni (vyote vipo Dar).
ASIMULIA VIPIGO, UKE WENZA
Mwanamke huyo aliweka hadharani kwamba mumewe amekuwa akimpiga mara kwa mara na tatizo kubwa ni uke wenza ambapo alidai ameoa mke wa pili hivi karibuni na mapenzi baina yao yamezorota.
“Mimi kabla ya kufunga naye ndoa Januari Mosi, 2013 mume wangu alikuwa na mke mwingine lakini aliamua kumpa talaka baada ya kumweleza kuwa mimi sitaki kuwa mke mwenza.

“Tukawa tunaishi naye lakini hata hivyo hakuchukua muda mgogoro ukaanza ndani ya nyumba.
Picha hii ikionyesha majeraha ya mkononi na shingoni aliyopata Bi. Nasra Dafa.


SAKATA LAFIKA KWA NDUGU


Mwanamke huyo aliendelea kusema kwamba hali ilizidi kuwa mbaya hadi ikafika kwa wana ndugu kwa suluhu, walipatanishwa lakini baada ya muda mgogoro ukaendelea na kuna siku mumewe akamwambia ameoa mke mwingine wiki tatu nyuma.
SIKU YA TUKIO

“Siku ya tukio, nilikuwa naswali. Unajua wakati wa Mfungo wa Ramadhani lazima Muislam kuswali kwa kuzingatia taratibu zote za dini. Basi, alikuja na kuniita nitoke nje lakini sikutoka.“Niliona nimalize kwanza kuswali  ndipo nitoke, lakini kabla sijamaliza akaja na kunishambulia kama niliovyokwambia kisha akachukua funguo na kufunga duka.
“Alipotoka hapo akaenda kwenye duka lingine la kuuza vocha nalo akalifunga na kuchukua fedha zote na kuondoka nazo huku muuzaji akiambiwa aende kwake,” alisema mwanamke huyo.

Amani lilifika kwenye Kituo cha Polisi Magomeni na kuambiwa na askari mmoja kuwa taarifa hizo zipo na mtuhumiwa anashikiliwa hapo, lakini akashauri atafutwe Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, ACP Camilius Wambura kwa maelezo zaidi. Kamanda huyo hakupatikana ofisini kwake hadi tunakwenda mtamboni.
SHEHE MKUU ASAKWA

Shehe Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Musa Salum hakupatikana kuzungumzia makosa ya mume wa Kiislamu kumpiga mkewe wakati akiswali ndani ya Mwezi Mtukufu.Hata hivyo,  Maalim Hassan Yahya Hussein wa Magomeni Mwembechai alipoulizwa alisema  Uislamu haujatoa ruhusa kwa mwanaume kumpiga mkewe wakati anaswali hata kama amefanya kosa kubwa kiasi gani.

“Uislamu haujaruhusu kwa hali yoyote udhalilishaji na kuna hadithi zinazokataza mtu kumdhuru mwenzake. Kuna masharti sita yamewekwa kabla ya mume kufikia hatua ya kumwadabisha mkewe,” alisema Maalim Hassan.Akaendelea: “Kabla mume hajampa adhabu mke anapaswa kwanza kumpa nasaha kwa kosa alilotenda na sharti la pili ni kumpa mawaidha ama yeye mwenyewe au atafute mtu.

“Sharti la tatu ni kumkumbusha mara kwa mara na  sharti la nne ni kumhama malazi, yaani kumuacha alale peke yake. Sharti la tano, akikosa ni kwenda kushitaki kwa wazee au katika vyombo vya sheria ikiwemo kwa kadhi na viongozi wa dini.“Sita ndiyo kumpiga, lakini kipigo ambacho hakitamdhuru kwani hutakiwi kumpiga ukiwa na hasira.

Mbunge wa Vunjo, Augustino Mrema (TLP) amesema amejiandaa kuingia ‘vitani’ na Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia ambaye ametangaza kuwania ubunge katika jimbo hilo, mwaka 2015.

“Siogopi mtu yeyote. Nimejiandaa vilivyo kwa mpambano huu. Najivunia rekodi yangu nzuri ya utendaji wala sitishiki na wananchi wangu nimewauliza wameniambia nisihofu,” alisema Mrema.

Kwa mujibu wa Mrema, anaamini rekodi yake nzuri ya utendaji ndiyo itakayomuuza mwaka 2015 na kwamba, ni rekodi hiyo nzuri ndiyo iliyowafanya wananchi wa jimbo hilo wakamchagua mwaka 2010.

“Umesahau nilikuwa mbunge wa Moshi Vijijini wakati huo ikiwa ni pamoja na Vunjo? Rekodi yangu nilipokuwa naibu waziri mkuu inajieleza. Yeye (Mbatia) aje nimejiandaa kwa mpambano,” alisema.

Juzi, Mbatia ambaye pia ni mbunge wa kuteuliwa, alisema kwa sasa ameelemewa na maombi ya makundi mbalimbali ya jamii yakimtaka agombee ubunge katika jimbo hilo mwakani.

“Nimefuatwa mara kadhaa na viongozi wa dini wakiniomba nigombee tena 2015. Wapo wananchi wamenifuata hadi bungeni. Simu yangu imejaa meseji nyingi za kuniomba,” alisema Mbatia.

Mbatia ambaye pia ni mwenyekiti mwenza wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), aliwahi pia kuwa mbunge wa kwanza wa jimbo hilo chini ya mfumo wa vyama vingi mwaka 1995 hadi mwaka 2000.

“Hayo maombi ya wananchi siwezi kusema nawakatalia, mimi ni nani nikatae kuwatumikia Watanzania wenzangu? Niko tayari kuwatumikia ila wajue kwa sasa kuna mbunge,” alisema.

Mbatia aliongeza, “Natarajia kwenda Vunjo wakati wowote kuanzia leo ili nitoe jibu rasmi mbele ya Wanavunjo. Nashukuru kwa heshima hii waliyonipa. Naahidi sitawaangusha.

Wiki iliyopita, baadhi ya wananchi waliodai kuwawakilisha wenzao kutoka kata zote za jimbo hilo, walitoa tamko lililosomwa na Mathew Temu wakimtaka Mbatia agombee ubunge kupitia vyama vya NCCR, Chadema na CUF vinavyounda Ukawa. Katika tamko hilo, wananchi hao walisema rekodi ya Mbatia alipokuwa mbunge haijawahi kuvunjwa.

Taarifa ya jeshi la polisi mkoa wa mbeya kwa vyombo vya habari “press release” tarehe 31.07.2014.

    Watu wanne wafariki dunia na wengine 51 kujeruhiwa katika ajali ya gari matundasi wilayani chunya.

    Mtu mmoja afariki dunia katika ajali ya barabarani jijini mbeya.

    Mtoto wa miaka mitatu afariki dunia baada ya kuangukiwa na kifusi cha mchanga wilayani chunya.

    Mtoto wa miaka kumi afariki dunia baada ya kupigwa na shoti ya umeme.

Katika tukio la kwanza:
 Watu wanne waliotambulika kwa majina ya 1. paulo mwasanga (18) mkazi wa kitongoji cha matundasi ‘b’ 2. wedi angolwise (21) mkazi wa matundasi 3. salome mwakibete (13) mwanafunzi wa darasa la saba shule ya msingi sambilimwaya na 4. obedi mwakamela (25) mkazi wa matundasi wamefariki dunia papo hapo baada ya gari lenye namba za usajili t.595 chu aina ya fuso tipper likiendeshwa na dereva asiyefahamika jina kipinduka katika kijiji cha matundasi wilayani chunya.
Ajali hiyo ilitokea mnamo tarehe 30.07.2014 majira ya saa 16:00 jioni huko katika kitongoji cha matundasi “b”, kijiji cha matundasi, kata ya matundasi, tarafa ya kiwanja, wilaya ya chunya, mkoa wa mbeya katika barabara ya chunya/makongolosi.

 gari hilo lilikuwa likitokea kijiji cha sambilimwaya kuelekea kijiji cha matundasi likiwa limebeba wachezaji wa mpira wa miguu na mashabiki. aidha katika ajali hiyo watu 51 walijeruhiwa, kati yao 26 walitibiwa na kuruhusiwa na wengine 25 wamelazwa katika hospitali ya wilaya ya chunya wakiendelea kupatiwa matibabu. chanzo cha ajali ni mwendo kasi, dereva alikimbia mara baada ya tukio na juhudi za kumtafuta zinaendelea.
 kaimu kamanda wa polisi mkoa wa mbeya kamishna msaidizi wa polisi barakael .n. masaki anatoa wito kwa madereva kuwa makini wanapotumia vyombo vya moto hasa kwa kuzingatia sheria na alama za usalama barabarani ili kuepuka ajali zinazoweza kuepukika. aidha anatoa wito kwa yeyote mwenye taarifa za mahali alipo mtuhumiwa azitoe katika mamlaka husika ili akamatwe na hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yake.

 katika tukio la pili:
 mtu mmoja aliyetambulika kwa jina la wile peter ambaye alikuwa abiria katika pikipikiamefariki dunia baada ya gari lenye namba za usajili dfp 0036 aina ya benz mali ya shirika la umeme tanesco lililokuwa  likiendeshwa na patrick mhagama (46) mkazi wa ilomba jiji mbeya kumgonga mpanda pikipiki asiyefahamika jina wala makazi yake na kusababisha kifo kwa abiria huyo.

 Ajali hiyo imetokea mnamo tarehe 31.07.2014 majira ya saa 16:45 jioni huko nzovwe, kata ya nzovwe, tarafa ya iyunga, jiji na mkoa wa mbeya. chanzo cha ajali kinachunguzwa. dereva amekamatwa na gari lipo kituoni. mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali ya rufaa mbeya.
 Kaimu kamanda wa polisi mkoa wa mbeya kamishna msaidizi wa polisi barakael .n. masaki anatoa wito kwa madereva kuwa makini wanapotumia vyombo vya moto hasa kwa kuzingatia sheria na alama za usalama barabarani ili kuepuka ajali zinazoweza kuepukika.

 Katika tukio la tatu:
 Mtoto mwenye umri wa miaka mitatu aliyetambulika kwa jina la pascalia jifula ngasa amefariki dunia baada ya kuangukiwa na kufunikwa na kifusi cha mchanga katika kitongoji cha chizya wilayani chunya.

 Tukio hilo limetokea mnamo tarehe 30.07.2014 majira ya saa 08:300 asubuhi huko katika kitongoji cha chizya, kijiji cha mwambani chini, kata ya mwambani, tarafa ya kwimba, wilaya ya chunya, mkoa wa mbeya. wakati tukio hilo linatokea, mtoto huyo alikuwa akicheza na watoto wenzake kwenye gema la mchanga na ndipo kifusi kumuangukia na kumfunika.

 Kaimu kamanda wa polisi mkoa wa mbeya kamishna msaidizi wa polisi barakael .n. masaki anatoa wito kwa wazazi na walezi kuwa makini na watoto wadogo kwa kuangalia mazingira ya maeneo yao ili kuepuka madhara yanayoweza kujitokeza.

 katika tukio la nne:
 Mtoto wa miaka kumi aliyefahamika kwa jina la jerry jested, mwanafunzi na mkazi wa mlowo wilayani mbozi alikutwa amekufa chumbani kwake baada ya kupigwa na shoti ya umeme.

 Tukio hilo limetokea mnamo tarehe 30.07.2014 majira ya saa 06:00 asubuhi huko katika kata ya mlowo, tarafa ya vwawa, wilaya ya mbozi, mkoa wa mbeya. inadaiwa kuwa chanzo cha tukio hilo ni baada ya marehemu kulamba nyaya za umeme ambazo zilikuwa karibu na kitanda chake hali iliyopelekea kupigwa shoti na kusababisha kifo chake.

 Kaimu kamanda wa polisi mkoa wa mbeya kamishna msaidizi wa polisi barakael .n. masaki anatoa wito kwa wazazi na walezi kuwa makini na watoto wadogo kwa kuangalia mazingira ya maeneo yao ili kuepuka madhara yanayoweza kujitokeza ikiwa ni pamoja na kuweka mbali vitu vya hatari kwa watoto.
 imetolewa na kusainiwa na:
 [barakael .n. masaki – acp]
kaimu kamanda wa polisi mkoa wa mbeya.

Wednesday 30 July 2014


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete kwa mara nyingine ametunukiwa tuzo la kimataifa – zamu hii kwa kuwa mshindi waTuzo la Nyota wa Demokrasia Afrika  2014 – Icon of Democracy Award Winner for 2014 in Africa.

Kwa mujibu wa barua aliyoandikiwa Rais Kikwete na kupokelewa Ikulu, Dar Es Salaam, Rais Kikwete amekuwa mshindi wa kwanza, na kwa mbali kabisa, katika mchuano na marais watatu wa Afrika ambao walifikia mwisho mwa mchuano wa kuwania tuzo hilo.

Katika barua hiyo, Mchapishaji na Mhariri Mkuu wa Jarida hilo, Pastor Elvis Iruh, akizungumza kwa niaba ya Kamati ya Tuzo 2014, amesema kuwa uongozi wa Rais Kikwete umekuwa ni hadithi ya kusifiwa ya mafanikio katika Bara ambako hadithi za namna hiyo siyo nyingi.

Tuzo hilo hutolewa na Jarida la The Voice na mwaka jana mshindi alikuwa ni Rais Bai Koroma wa Sierra Leone ambaye alikuwa ni mshindi wa pili wa Tuzo hiyo ambalo ilitolewa kwa mara ya kwanza kwa Rais wa Kwanza wa Zambia, Mzee Kenneth Kaunda.

Sherehe maalum ya kukabidhi tuzo hiyo imepangwa kufanyika Oktoba 17, mwaka huu, 2014, katika Hoteli ya Van der Valk, iliyoko Almere, Uholanzi.

Miongoni mwa sifa nyingine, Rais Kikwete anatunukiwa Tuzo hiyo kwa sababu ya kuwa msimamizi mzuri na wa kweli wa demokrasia, kuendelea kuhakikisha kuwa amani, utulivu na maendeleo vinaendelea kupatikana katika eneo la Afrika ambalo limepitia vipindi vingi vya migogoro na matatizo.

Aidha, gazeti hilo linasema kuwa Rais Kikwete amekuwa kiongozi wa mfano, kimataifa na kikanda, na linatoa mfano wa mchango wake katika kusuluhisha mgogoro mkubwa wa kisiasa nchini Kenya kufuatia uchaguzi mkuu wa 2007.

Rais Kikwete pia anasifiwa kwa mchango wake katika kusimamia maendeleo ya Tanzania katika nyanja mbali mbali – kilimo, elimu, miundombinu, maendeleo ya viwanda, utalii na pia mchango wake katika kuendeleza vijana na kutoa nafasi nyingi kwa akinamama kushika nafasi nyingi za uongozi.

Jarida la The Voice pia limempongeza Rais Kikwete kwa kuimarisha Umoja na Muungano wa Tanzania na kutoa nafasi kwa wananchi kujadili na kukubaliana kuhusu Katiba mpya ya Tanzania.

Aprili mwaka huu, Rais Kikwete alitunukiwa tuzo la kuwa kiongozi mwenye mchango mkubwa zaidi katika maendeleo ya Afrika kwa mwaka 2013 – The Most Impactful Leader in Africa 2013.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu – Dar es Salaam.
30 Julai,2014

 

Takribani watu 20 wanadaiwa kupoteza maisha huku wengine wengi wakijeruhiwa baada ya basi la Moro Best lililokuwa linatoka Mpwapwa kwenda Dar es Salaam kugongana uso kwa uso na lori eneo la Pandambili, Kongwa mkoani Dodoma leo. Baadhi ya majeruhi wa ajali hiyo wamepelekwa katika Hospitali ya Mkoa Dodoma huku wengine wakipelekwa Hospitali ya Mpwapwa.





Ziwa Nyasa limezungukwa na nchi tatu ambazo ni Tanzania,Malawi na Msumbuji.Ziwa hilo lipo kwenye usawa wa meta 500 toka usawa wa bahari, kina cha ziwa hilo ni karibu meta 750,urefu wake ni karibu  kilometa 1000,upana mkubwa ni kilometa 80 na upana mdogo ni kilometa 15.Huku tafiti mbalimbali zikionesha kuwa ziwa hulo ndilo zuwa pekee linaongoza kwa aina za samaki ,na kutokana na utafuti ambao umefanyika katika ziwa Nyasa upande wa Tanzania na Malawi umebaini kuwa ziwa hilo linaoongoza ulimwenguni kwa kuwa na aina nyingi za samaki ukilinganisha na maziwa mengine duniani.

Kulingana na utafiti ambao ulifanywa na jumuiya ya nchi zilizo kusini mwa Afrika(SADC) kwa kushirikiana na  nchi ya Uingereza kwenye ziwa Nyasa kati ya mwaka 1991 hadi 1994 na mwaka 1996 hadi 2000,ulionesha kuwa ziwa hilo lina kiasi cha tani 165,000 za samaki na kati ya kiasi hicho tani 35,000 za samaki ni jamii ya samaki wa maji ya juu ambao wanaweza kuvuliwa bila kuathiri uvuvi kila mwaka. 

Licha ya tafiti hizo lakini wavuvi wa mwambao huo hawana Kikosi cha Polisi cha Wanamaji wa kuweza kusaidia uokozi wa majanga yanayotokea Ziwani.PITIA BAADHI YA PUCHA HIZI.

Hiyo ni hali halisi kwa Wakazi wa Mwambao wa Ziwa Nyasa wanavyokabiliana na hali ya Majanga yanayotokea Ziwani, hakuna Uokozi wa uhakika bali kutumia zana za Asili katika kuwaokoa watu wanaopatwa na majanga katika Ziwa Nyasa.
Vijana wa uokoaji katika Mwambao wa Ziwa Nyasa wakitoka kuwaokoa Vijana wawili waliozama kwenye Maji, Yohana Behewa na john Behewa waliozama Kilindini kilometa 20 kutoka nchi kavu katika maeneo ya Kijiji cha Chiulu Wilaya ya Nyasa Mkoani Ruvuma .
Vijana wa Uokozi wakivuta Mtumbwi uliowaokoa vijana waliokuwa wamezama kutokana na kupigwa na Wimbi wakati wa Dhoruba kali wakati wakiwa Ziwani.
Hapo ni vijana waliookolewa wakiwa wamefikishwa Nchi kavu ambako walipatiwa msaada baada ya kuokolewa na vijana wenzao huku wakiwa wamechoka kutokana na kunywa  maji.
Kikosi cha ukoaji Kilichopo Kijiji cha Chiulu wakivuta mtumbwi uliobeba watu waliowakoa kutoka Ziwani baada ya kupigwa na dhoruba na kuzama majini hali iliyotokana na matumizi ya Zana hafifu ambazo hazikidhi kwa kushindana na Mawimbi makali yanayo tokana baada ya  Dhoruba kali  inapotokea katika Mwambao wa Ziwa Nyasa. Wananchi wa Mwambao wa Ziwa Nyasa wamesema hali hiyo imekuwa ikitokea mara kwa mara na hakuna njia nyingine inayotumika kuokoa wahanga wanaopatwa na kadhia hiyo zaidi ya kutumia vifaa duni walivyonavyo.

article-2710210-201DD49500000578-25_634x414

Shinji Kagawa, Darren Fletcher na Tom Cleverley, wafungaji wanne wa penati za United, wakishangilia ushindi wao wa penalti 5-3 dhidi ya Inter Milan.
article-2710210-201DD4F500000578-474_634x417
Fletcher akishangilia ushindi na kipa wa United David De Gea baada ya kushinda kwa penalti na kumpa Van Gaal rekodi ya ushindi wa asilimia 100 katika michuano hiyo.
KOCHA Louis van Gaal ameendelea kufanya vizuri kufuatia Manchester United kuitandika kwa penalti 5-3 Inter Milan baada ya sare ya 0-0 katika mechi ya Kombe la Kimataifa kujiandaa na msimu mpya nchini Marekani.

Katika mchezo huo uliofanyika kwenye Uwanja wa FedEx Field mjini Washington, penati za Man United zilizamishwa kambani na Ashley Young, Javier Hernandez, Tom Cleverley, Shinji Kagawa na Darren Fletcher wakati Marco Andreolli wa Inter aligongesha mwamba. 
ziara hiyo ya Marekana imekuwa ya mafanikio kwa Van Gaal kwani ameshinda mechi tatu mfululizo na wachezaji wake wamepata nafasi ya kumuonesha uwezo, hivyo lawama hazitegemewi.

Kocha huyo mpya wa United anaendelea kutafuta njia ya kuutekeleza mfumo wake anaoupenda wa 3-5-2.

Kwa mfano jana usiku, Man United walianza mchezo na washambuliaji wawili,  Wayne Rooney na Danny Welbeck. Walimaliza mchezo na Nani na Wilfried Zaha katika nafasi hizo.

TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA VYOMBO VYA HABARI
“PRESS RELEASE” TAREHE 30.07.2014

MMG23716
[BARAKAEL .N. MASAKI – ACP]
  • MZEE WA MIAKA 75 AUAWA KWA KUKATWA NA KITU CHENYE NCHA KALI NA MTU/WATU WASIOFAHAMIKA.
  • MTEMBEA KWA MIGUU AFARIKI DUNIA KATIKA AJALI YA MAGARI MAWILI KUGONGANA.
 KATIKA TUKIO LA KWANZA: 
MZEE MMOJA MWENYE UMRI WA MIAKA 75 ALITAMBULIKA KWA JINA LA DAIMONI MATATA, MKAZI WA KIJIJI CHA LUSINGO ALIUAWA KWA KUKATWA NA KITU CHENYE NCHA KALI SEHEMU ZA SHINGONI NA MTU/WATU WASIOFAHAMIKA.
TUKIO HILO LIMETOKEA USIKU WA KUAMKIA LEO MAJIRA YA SAA 02:00 HUKO KATIKA KIJIJI CHA LUSINGO, KATA YA SONGWE, TARAFA YA BONDE LA USONGWE, WILAYA YA MBALIZI, MKOA WA MBEYA. CHANZO CHA TUKIO HILO BADO KINACHUNGUZWA. AIDHA MTU MMOJA AMBAYE NI MTOTO WA MAREHEMU AITWAYE WATSON DAIMONI (53) MKAZI WA KIJIJI CHA LUSINGO AMEKAMATWA KWA MAHOJIANO KUHUSIANA NA TUKIO HILI.
MWILI WA MAREHEMU UMEHIFADHIWA KATIKA HOSPITALI TEULE YA IFISI – MBALIZI KWA UCHUNGUZI WA KITABIBU. UPELELEZI ZAIDI JUU YA TUKIO HILI UNAENDELEA.
 KAIMU KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI BARAKAEL .N. MASAKI ANATOA WITO KWA YEYOTE MWENYE TAARIFA ZA MTU/WATU WALIOHUSIKA NA TUKIO HILI AZITO KATIKA MAMLAKA HUSIKA ILI HATUA ZA KISHERIA ZICHUKULIWE DHIDI YAO. AIDHA ANASHAURI FAMILIA ZIWE NA UTAMADUNI WA KUKAA NA KUTATUA KERO NA CHANGAMOTO MBALIMBALI AMBAZO ZINAJITOKEZA KATIKA KAYA ZAO ILI KUEPUKA MADHARA/MATATIZO YANAYOWEZA KUJITOKEZA.
 KATIKA TUKIO LA PILI:
 MTEMBEA KWA MIGUU MMOJA ALIYETAMBULIKA KWA JINA LA BARAKA ZAWADI MJEMWA (31) MFANYABIASHARA NA MKAZI WA MIKOROSHINI – KYELA AMEFARIKI DUNIA BAADA YA GARI LENYE NAMBA ZA USAJILI T.604 BCS AINA YA TOYOTA NOAH LIKIENDESHWA NA DEREVA AITWAYE ASAJILE AYUB (35) MKAZI WA KASUMULU KULIGONGA GARI JINGINE LENYE NAMBA ZA USAJILI T.649 ALB AINA YA TOYOTA HILUX LILILOKUWA LIKIENDESHWA NA DEREVA AITWAYE MUSA MWALUBANGE (32) MKAZI WA KIJIJI CHA MBUGANI NA KISHA KUPOTEZA MWELEKEO NA KUMGONGA MTEMBEA KWA MIGUU HUYO.
 TUKIO HILO LIMETOKEA MNAMO TAREHE 29.07.2014 MAJIRA YA SAA 12:00 MCHANA HUKO KATIKA KIJIJI CHA ILAMBO, KATA YA ITOPE, TARAFA YA UNYAKYUSA, WILAYA YA KYELA, MKOA WA MBEYA. CHANZO CHA AJALI NI BAADA YA GARI T.604 BCS KUTAKA KUYAPITA MAGARI YALIOKUWA MBELE YAKE BILA KUCHUKUA TAHADHARI. DEREVA AMEKAMATWA.
 KAIMU KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI BARAKAEL .N. MASAKI ANATOA WITO KWA MADEREVA KUWA MAKINI WANAPOTUMIA VYOMBO VYA MOTO HASA KWA KUZINGATIA SHERIA NA ALAMA ZA USALAMA BARABARANI ILI KUEPUKA AJALI ZINAZOWEZA KUEPUKIKA.
 Imetolewa na kusainiwa na:
[BARAKAEL .N. MASAKI – ACP]
KAIMU KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.


















Mrembo almaarufu kwa jina la 'Winnie Mandela' katika muziki wa kizazi kipya akiwa amenaswa na polisi China.
HUKU modo maarufu Bongo, Jacqueline Fitzpatrick Cliff ‘Jack Patrick’, akisota jela nchini China kwa skendo ya kukamatwa na madawa ya kulevya (unga), mrembo mwingine ambaye aliwahi kujaribu kuchomoka kisanii kwenye muziki wa Kizazi Kipya almaarufu kwa jina la Winnie Mandela, naye amenaswa na polisi nchini humo.
Tukio hilo lilijiri mwishoni mwa wiki iliyopita baada ya kupitishwa kwa msako maalum wa kutokomeza biashara hiyo katika viunga vya Mji wa Hong Kong, China. 

JUX, PETIT MAN WAPATA WAKATI MGUMU
Kwa mujibu wa chanzo chetu chenye maskani yake Hong Kong, Mbongo Fleva, Juma Khaleed ‘Jux Vuitton’ na meneja wa msanii wa Bongo Fleva aitwaye Mirrow, Petit Man nao walijikuta kwenye wakati mgumu baada ya kunusurika kuunganishwa kwenye oparesheni hiyo ya ukamataji wa waingizaji wa madawa ya kulevya nchini China.

'Winnie Mandela' wa muziki wa kizazi kipya Bongo akiwa chini ya ulinzi mkali China.

MADAI YA KUBEBA UNGA
Ilidaiwa kwamba Winnie alijikuta mikononi mwa askari wa China akidaiwa kubeba mzigo wa unga tumboni hivyo kukamatwa na kutembezwa mitaani kuelekea kituo cha polisi. 

APITA VIZUIZI, AKAMATWA
Ilisemekana kwamba Winnie ambaye ni msichana wa mjini Dar, alifanikiwa kupita vizuizi vyote lakini kwa hali ilivyo kwa sasa nchini humo ndipo akajikuta akikamatwa na kutembezwa mtaani kama mhalifu wa kivita.
“Unaambiwa ilikuwa kama vita kwani polisi wa China huwa wana silaha za kutisha sana. Unajua Winnie alikamatwa kwenye mitaa ambayo kuna Wabongo wengi hapa Hong Kong,” kilisema chanzo chetu kutoka Hong Kong.
Ilidaiwa kwamba askari hao walipokea agizo maalum kutoka kwenye kitengo cha kudhibititi madawa ya kulevya nchini humo kwani kwa sasa nchi hiyo imechafuka kwa uingizwaji wa madawa ya kulevya, jambo ambalo limeifanya serikali ya China ifanye oparesheni kubwa ya kuhakikisha wanatokomeza wimbi hilo. 

KWA WABONGO CHINA

Chanzo chetu kilisema kwamba kwa sasa Wabongo wanaokwenda au wanaokaa China wanaishi kama digidigi kwani wamefikia hatua ya kutoonesha pasipoti  zao na hata wengine wanadiriki kukataa uraia wao kwa kuwa Wabongo ndiyo wanasakwa kwa wingi.
“Sasa hivi jamaa wakisikia huyo ni Mtanzania wanamfuatilia sana kwani ndiyo wenye sifa ya uingizaji wa dawa za kulevya nchini China,” kilisema chanzo hicho na kuongeza:

KAMA HUAMINI MUULIZE JUX AU PETIT MAN
“Hicho ndicho kilichomtokea Winnie. Nakwambia Wabongo wanazidi kukamatwa na madawa ya kulevya. Yaani ni aibu, huwezi kuamini.
“Wabongo wengi sana wamekamatwa Hong Kong na wengine familia zao Bongo hazijui.
“Kama Watanzania hawaamini wawaulize Jux na Petit Man ambao walishuhudia mtiti mwanzo mwisho.” 

BALOZI WA TANZANIA CHINA
Ili kupata undani na idadi ya Watanzania wanaokamatwa kwa ishu za madawa ya kulevya nchini China, gazeti hili lilimtafuta Balozi wa Tanzania China, Luteni General Abraham Shimbo ambapo simu yake ya ofisini iliita bila kupokelewa. Wakati Jack Patrick akisubiri kupandishwa kizimbani kwa mara nyingine mwezi ujao, ripoti zinaonesha kwamba wapo Watanzania wengi waliofungwa na wengine kunyongwa kwa msala wa madawa ya kulevya.

Katibu wa CHADEMA Wilaya ya Ubungo, Goodluck JustineUONGOZI mpya wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo wilaya ya kichama Ubungo unatarajiwa kujulikana Agosti 3 mwaka huu baada ya uchaguzi wa ngazi za chini katika wilaya hiyo kukamilika.

Mbali na viongozi wa wilaya hiyo kujulikana siku hiyo, pia chama hicho kimeeleza kuwa, kimejiandaa vema kuwadhibiti mamluki wasijipenyeze katika uongozi huo.

Hayo yalibainishwa na Katibu wa CHADEMA Wilaya ya Ubungo, Goodluck Justine, wakati akielezea mafanikio yaliyopatikana katika uchaguzi wa ngazi za msingi, matawi na kata.

Justine alisema, ni fursa kwa kila mwanachama muadilifu wa CHADEMA Wilaya ya CHADEMA Ubungo kuwania nafasi anayoona ataimudu.

Aliongeza kuwa, katika uchaguzi wa ngazi za chini, chama hicho kimefanikiwa kujiimarisha na kuongeza wanachama zaidi.

Alisema, fomu zimeanza kutolewa jana na mwisho wa kuchukua na kurejesha itakuwa Agosti Mosi saa 10 jioni