Tuesday 23 September 2014

            

1_797b9.jpg
2_755c0.jpg
3_bbf6d.jpg
4_ab685.jpg
005_3863f.jpg
05_96e9e.jpg
5_5a7af.jpg
15_b219c.jpg
16_858ae.jpg
17_39785.jpg
18_6193f.jpg
20_c755e.jpg
21_e531c.jpg
22_9ac88.jpg
23_5a695.jpg
24_2ec26.jpg
25_c0154.jpg
26_10fb0.jpg


  Mbunge wa jimbo la Temeke na Mwenyekiti wa Wabunge Mkoa wa Dar es Salaam Abbas Mtemvu akiwa anaingia  Ofisi ya katibu kata,ya chama cha Mapinduzi CCM Buza Dar es Salaam
 Mbunge wa jimbo la Temeke na Mwenyekiti wa Wabunge Mkoa wa Dar es Salaam Abbas Mtemvu akitia saini katika kitabu cha wageni Ofisi ya katibu kata ya chama cha Mapinduzi  CCM Buza Dar es Salaam.
 Mbunge wa jimbo la Temeke na Mwenyekiti wa Wabunge Mkoa wa Dar es Salaam, Abbas Mtemvu,(wapili kulia) wakipiga makofi wakiimba wimbo wa chama hicho mara alipo wasili Ofisini hapo,kuanzia kushoto ni Mwenyekiti UVCCM kata ya Buza,Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana Jimbo la Temeke na msaidizi wa Mbunge wa jimbo hilo upande wa Vijana.Peter Sillo,aliye vaa shati la kijani ni  Mwenyekiti wa CCM kata ya Buza, Shabani Bambo  na wakwanza ni Katibu kata ya Buza Shabani Abdallah.
 Katibu kata ya Buza Shabani Abdallah, akimkaribisha Mgeni rasmi Mbunge wa Jimbo la Temeke Abbas Mtemvu, na akitambulisha  katika hafla fupi ya kukabidhi jezi na pesa taslim kwa  matumizi mbalimbali ya kiofisi, katika moja ya ahadi aliyoitowa kwa majimbo matano kwa wanachama wa chama cha Mapinduzi(CCM) Buza.
 Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Temeke (CCM),Ally Mehalla ,akisalimia wanachama wa chama hicho
 msaidizi wa Mbunge wa jimbo la Temeke upande wa Vijana.Peter Sillo kushoto akisalimia wanachama wa chama cha Mapinduzi (kushoto) Mwenyekiti wa( CCM)  kata ya Buza, Shabani Bambo anaye fatia ni Mbunge wa jimbo la Temeke Abbas Mtemvu na kulia ni Katibu kata ya Buza Shabani Abdallah.
 Viongozi wa Matawi kata ya Buza
 Mbunge wa jimbo la Temeke na Mwenyekiti wa Wabunge Mkoa wa Dar es Salaam Abbas Mtemvu(kulia), akikabidhi Pesa Taslim kwa katibu wa Uchumi wa chama hicho Hawa Zuberi, kwa matumizi mbalimbali ya kata ya Chungu Buza Dar es Salaam.
Mbunge wa jimbo la Temeke na Mwenyekiti wa Wabunge Mkoa wa Dar es Salaam Abbas Mtemvu(kulia) akimkabidhi Jezi na pesa taslim katibu wa Tawi la Mashine ya Maji5 Baraka Mohamedi
 Mbunge wa Jimbo la Temeke na Mwenyekiti wa Wabunge  Mkoa wa  Dar es salaam,Abbas Mtemvu (kulia),akimkabidhi Mwenyekiti wa CCM kata ya Buza seti ya Jezi pamoja na Pesa taslim Sh.milioni moja na laki moja.  Johari Mkonde (kushoto), kati ya ahadi aliyoitowa kwa majimbo matano kwa wanachama wa chama cha Mapinduzi . anaye shuhudia ni Mwenyekiti wa chama hicho kata ya buza, Shabani Bambo.
 Mbunge wa Jimbo la Temeke akitoka na viongozi kwanda eneo lililo haribiwa na Mvua na kusababisha njia hiyo kutopitika na Magari yakawa hayapiti katika njia hiyo, kati ya Vituka Machimbo na Buza Shule na jinsikani wataweza kuweka Daraja katika Mto wa Buza ili wanafunzi na wananchi waweze pita kwa urahisi kutokana na ukaribu wa eneo hilo.
 Wakiwa katika kituo kidogo cha Polisi cha Buza ,kujionea maendeleya ya kituo hicho baada ya kutoa Pesa awamu ya kwanza na kuahidi kukimalizia na kuwawekea Fenicha mbalimbali kituoni hapo.
Njia iliyo haribiwa na Mvua na Gari kuto pita tena
 
 
 
 
 
 

Monday 22 September 2014


 Warembo 15 kati ya 30 wanaoshiriki shindano la Redds Miss Tanzania 2014 wakisindikizwa na mkali wa Bongo Fleva kutoka Jijini Dar es Salaam, Tunda Man, wametoa burudani kali wakati wa shindano dogo la awali la kumtafuta mrembo mwenye kipaji lililofanyika Babati Mkoani Manyara. Pichani juu ni washindi wa tano waliofanikiwa kuingia fainali ya shindano hilo la vipaji litakalofanyika jijini Dar es Salaam baada ya wengine 15 kufanyika Arusha mjini. 
 Warembo hao walishindana vikali katika kucheza na kuimba miziki ya aina mbalimbali.
 Jopo la majaji likifuatilia kwa makini shindano hilo
 Kila aina ya stile za uchezaji zilioneshwa na warembo hao jukwaani…

 wadau wa sanaa ya Urembo Babati wakifuatilia shindano hilo.
Mkuu wa Wilaya ya Hanang, Christina Mndeme aliye mwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Manyara, akiwa na waratibu wa show hiyo, Mzee Ally Sumaye (kushoto) na Mfanyabiashara Mohamad Bajwa.
 Msanii wa Bongo Fleva  Tunda Man akitoa burudani kwa wadau wa urembo Babati.

Friday 19 September 2014


Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu, akizungumza na waendesha pikipiki (Maarufu kama  Boda Boda) leo katika ukumbi wa Songea Club uliopo Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma. Mwambungu amewataka madereva Boda boda kuepusha ajali za barabarani kwa kufuata sheria, na kutotumiwa na vyama vya kisiasa.



BAADA ya siku chache kupita kufuatia tukio la nani amefanya kitendo kiovu cha kurusha bomu la kienyeji katika mtaa wa Msufini Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma, na kujeruhi baadhi ya askari Polisi mjini hapa, Mkuu wa mkoa huo Said Mwambungu amekutana na waendesha pikipiki wa manispaa hiyo na kuwataka  kujenga ushirikiano ili kuweza kulinda amani ya nchi dhidi ya maadui ambao hawalitakii mema taifa hili.
Mwambungu amekutana leo na madereva hao maarufu kwa jina la “Boda boda” katika ukumbi wa Songea Club uliopo mjini Songea, akisisitiza kujenga ushirikiano kwa vyombo vya usalama ili kuweza kupata ukweli wa tukio hilo na kuwafanya wakazi wa mji huo, watu wengine (wageni) wanaoingia na kutoka kuondoa hofu na kuishi katika hali ya usalama.
Akizungumza kwa njia ya simu na mwandishi wa habari hizi, Mkuu huyo wa mkoa alisisitiza kuwa jamii ihakikishe kwamba amani utulivu vinatawala miongoni mwao, na pale wanapoona kuna sintofahamu ni vyema watoe taarifa katika vyombo husika vya usalama ili kuweza kubaini uhalifu unaofanyika na hatua ziweze kuchukuliwa haraka dhidi ya wahalifu.

“Ni kweli leo nimezungumza nao, ni kawaida yangu kukutana nao jambo kuu nimesisitiza kujenga ushirikiano na  amani, na waache kutumiwa katika mambo ya kisiasa, siku zote amani ndio msingi mkuu”, alisema Mwambungu.
Mwambungu aliongeza kuwa hivi sasa vyombo vya ulinzi na usalama vinaendelea na uchunguzi juu ya tukio hilo, na kwamba mpaka sasa hakuna mtu aliyepatikana ambaye anahusika kutenda unyama huo.
Pamoja na mambo mengine tukio la kurushwa kwa bomu hilo, lilitokea Septemba 16 mwaka huu majira ya 1:25 usiku katika mtaa wa Msufini katika Manispaa ya Songea na kuwajeruhi askari Polisi watatu kati ya w anne waliokuwa doria huku Jeshi la Polisi nchini likithibitisha kuwa bomu hilo limetengenezwa kienyeji.
Askari waliojeruhiwa ni G 5515 PC John, G 7351 PC Ramadhan na WP 10399 Felista ambapo baada ya kujeruhiwa kwa bomu hilo, walikimbizwa katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Ruvuma kwa ajili ya matibabu zaidi.

PC John aliyepata majeraha kiasi alipatiwa matibabu siku hiyo na kuruhusiwa, huku askari wawili PC Ramadhan na WP Felista wakiendelea kupatiwa matibabu hospitalini hapo.