Friday 19 December 2014


Kwa nchi nyingi za Afrika hasa Tanzania zinapiga marufuku kubwa ya uonyeshwaji wa movie za ngono kutokana na kwamba hazina maadili mazuri kwenye jamii, ukienda nchi kama China wao wameenda mbali zaidi, sheria kali zimewekwa ili kuzuia kabisa mtu yeyote kucheza filamu hizo, ama kuuza.

Nchi za Ulaya na Marekani zimekuwa zikishutumiwa kuruhusu biashara zote, kutengeneza na kuuza movie hizo, lakini hii kutoka Los Angeles, Marekani imeweka sheria inayowalazimu waigizaji wa filamu hizo za ngono kuvaa mipira maalum ya kuwakinga na maambukizi ya magonjwa, Condom.

Sheria hii ambayo iliyoanza kama muswada mwaka 2012 inawalazimu waandaaji wa filamu hizi pia kulipia ada maalum ili kupewa kibali cha kufanyia kazi hiyo.

Waandaaji wengi wa filamu za ngono wamelalamikia sheria hii wakidai kuwa inakwenda kinyume na haki zao za msingi japo Mahakama imetoa tayari msimamo wake.

Wadau wa industry ya filamu hizo wamedai kuwa wanafahamu fika hatari zilizoko kwenye maambukizi na wanachukua hatua za kupunguza maambukizi haya kwa kuwakinga na kuwapima watu wote wanaoshiriki uigizaji wa filamu hizi kabla ya kuingia nao mikataba ambapo utaratibu huu mpya unawapa hofu waandaaji hao kwamba huenda soko la biashara yao likayumba

0 comments:

Post a Comment