Wednesday 31 December 2014

Rais Jakaya Kikwete

















PANAPO MAJAALIWA ya Mungu, kesho tunaungana na mataifa mengine duniani kusheherekea mwaka mpya wa 2015.
Hivyo, kwa hesabu za kalenda ya mwaka 2014, leo hii tunamaliza muda uliobaki kabla ya kuingia mwaka 2015.
Tuna kila sababu ya kumshukuru Mungu kwa kuendelea kutupa pumzi yake. Ametujaalia afya njema. Hili ni jambo la kushukuru.
Pia nitumie nafasi hii kutoa pole kwa ndugu, rafiki na jamii zetu ambao leo hii hatunao tena. Wametangulia mbele za haki.
Hiyo inatokana na mapenzi yake muumba wa mbingu na ardhi. Tuwaombee dua njema huko waliko.Mbele zao, nyuma zetu.
Wakati tunakaribia kuingia mwaka 2015, nitumie nafasi hii kuowambea wale wote wenye kusumbuliwa na magonjwa mbalimbali.
Imani yangu Mungu atawaponya na kuwarejesha kwenye afya njema na hatimaye kuendele na ujenzi wa taifa.
Wakati tunajiandaa kuupokea mwaka mpya, kuna mambo mengi ambayo yametokea kwenye mwaka huu wa 2014.
Yapo ambayo yametunufaisha kama taifa lakini wakati huo huo yapo ambayo yametufedhehesha.
Mwaka 2014 ulikuwa mwaka wa matukio mengi katika nyanja mbalimbali. Nikiri kuna mambo ya kujivunia na kuna mambo ya hovyo ambayo yametokea kwenye taifa hili ambalo linaendelea na juhudi za kusaka maendeleo yake.
Sote ni mashahidi Watanzania kwa nafasi zao mbalimbali wameendelea na ujenzi wa taifa leo. Wameendelea kudumisha umoja na mshikamano wao.
Wameendelea kuungana kupigania maisha yao. Ni watu ambao hawataki kukataa tamaa. Wanafanya kila juhudi kuhakikisha taifa linasonga mbele.
Nikiri kauli ambayo inaliumiza taifa hili ni kuendelea kuimba wimbo wa “Sisi maskini”. Wimbo ambao kwangu mimi unaniumiza kichwa. Sitaki hata kuusikia. Sitaki kuusikia kwasababu ni sehemu ya adui wetu wa maendeleo yetu.
Sisi maskini ni kauli ambayo imetukwamisha kwa miaka mingi sasa. Hata mwaka huu wa 2014, kauli ya sisi maskini imeturudisha nyuma.
Kujiita kila siku maskini ndio matokeo yake tunashinda kuishi maisha ya kuendelea kuomba misaada. Kisa tu nchi yetu eti maskini.
Kwangu naamini sisi si maskini ila huenda tunakosa mipango na usimamizi mzuri wa kufikia malengo yetu.hili ndilo tatizo ambalo linatusumbua kwa miaka mingi.
Mwaka 2015 ni mwaka wa kubadili mitazamo na fikra zetu. Tukitumia vema rasilimali zetu, tutapiga hatua. Kila kitu tunacho.tunachotakiwa ni mipango na usimamizi mzuri. Tuache akili za kuwa tegemezi kwa kila jambo.
Inashangaza tunapokuwa na msitu mkubwa wa misitu kama ule wa Sao hili Iringa halafu kijiti cha kusafishia meno kinatoka China. Ama kweli!
Inasikitisha kuona imefika mahali eti kila kitu lazima kitoke nje. Kasumba hii inatokana na yale yale ambayo wengi yametutawala kwenye akili zetu kuwa lazima tuwe tegemezi.
Hatupaswi kuwa na akili hiyo kwa mwaka 2015. Ni mwaka wa kutafakari kama taifa nini tufanye ili tusonge mbele.
Kwa bahati mbaya tumekuwa na kundi kubwa ambalo linatumia muda mwingi kupiga soga vijiweni kwa ajenda ambazo hazina mashiko ya kimaendeleo. Ni rahisi kusikia watu wanajadili nani kavaa nini. Fulani analula nini?
Wanaojadili tunapigaje hatua kama taifa ni wa chache. Hata hao tunaowategemea kutupigania wamekuwa wa kuishi kwa matukio. Likija tukio hili wamo, likija lingine wamo.Mafundi wa kuongoa kuliko kutenda.
Inasikitisha sana.Tumeyaona hayo mwaka 2014.Si vizuri yakajirudia tena mwaka 2015. Kufanya kosa si kosa ila kurudia kosa, ndio kosa. Tusimamie kama nchi tuangalie maisha yetu. Tumetoka wapi na tunakwenda wapi.
Tukisoma vitabu vya historia tunaambia Tanzania na China zilianza harakati za kusaka maendeleo mwaka mmoja. Nenda leo China kaingalie.
Hatufanani nayo kwa namna yoyote ile.Watu tulianza nao kwenye harakati za kutafuta maendeleo, eti leo tunawapigia magoti kuwaomba msaada.
Wachina wameijenga nchi yao.Wameamua kusimama kidete kuhakikisha taifa lao linapiga hatua na kuwa lenye nguvu duniani.  Sishangai Marekani inapokwenda kuomba misaada ya kifedha China.
Kwetu sisi maendeleo yetu yamekuwa ya mwendo wa kinyonga. Wananchi wamekata tamaa ya maisha. Kila kukicha wanasema afadhali ya jana. Ndio maisha ambayo tumeamua kuishi.
Imefika mahali Wachina wameamua kuja nchini kwetu na kufanya kazi ambazo tumeshindwa kuzifanya. Nenda Kariakoo jijini Dar es Salaam, Wachina wanauza maua.Wanauza karanga.
Inasikitisha inapofika mahali hata karanga tunashindwa kuuza. Tunasibiri Wachina waje wauze. Halafu tumebaki kupiga kelele tu.Tumefika mahali pabaya.
Sifa ya taifa kupiga hatua za maendeleo linahitaji kuwa na siasa safi, utawala bora, ardhi na watu.
Nikiri tunaweza kuwa tumekosa siasa safi na uongozi bora lakini tuna ardhi ya kutosha na watu. Kwa bahati mbaya watu wapo lakini kasi ya maendeleo haiendani na idadi yetu.
Kitendo cha kukosa siasa safi imefika mahali, wanasiasa wengi wametugeuza kama vile kichwa na mwendawazimu. Wanatuongopea watakavyo.
Wanajua hatuna tunaloweza kulifanya. Hakika mwaka 2014, licha ya kufanya mambo ya maendeleo, yapo ambayo tunapaswa kujiepusha nayo mwaka 2015.
Msomaji wa safu hii, baada ya kutoa maelezo hayo ambayo kwangu mimi kwa siku ya leo ni kama utangulizi sasa nije kwenye ajenda yangu ya Jumatano ya leo.
Ajenda yenyewe ni hili sakata la Escrow.Sakata ambalo limekuwa gumzo kwenye kila kona ya nchi yetu. Limekuwa likizungumza na kila mtu. Kama hulizungumzi wewe basi analizungumza mwenzio.
Sakata la Escrow limetikisa nchi yetu kwa sehemu kubwa. Sote tunafahamu mjadala huo wa Escrow unatokana na utata wa fedha wa sh. bilioni 306 zilizopo kwenye akaunti ya Tegeta Escrow, wajanja kuamua kuzichukua.
Wanasiasa wa kada mbalimbali wamekuwa wakilizungumza hilo kwa kina. Wamekuwa wakipambana kwa hoja. Wamekuwa wakijadili na kuelezea umma kuhusu fedha hizo.
Nikiri mwaka 2014, mjadala wa Escrow kwangu mimi naona ulikuwa ni mjadala uliochokuwa sehemu kubwa ya mazungumzo kuliko mijadala mingine.
Ni kweli kulikuwa na mjadala kuhusu Katiba mpya lakini ujio wa sakata la Escrow umefunika kabisa mazungumzo ya Katiba inayopendekezwa.
Kwa kuwa hata wanasiasa wetu nao wanaishi kwa matukio. Wengi wao wameachana na ajenda ya Katiba mpya ambayo wananchi wanahitaji kuelimisha licha ya wao wenyewe kujisomea Katiba inayopendekezwa kabla ya kufanya uamuzi kwa kupiga kura ya ndio au hapa.
Leo hii ili mwanasiasa aonekane amezungumza jambo la maana basi anaamini akizungumzia Escrow ndio nyota ya siasa inasafishika.
Sina tatizo na wanasiasa ambao wamelizungumzia sakata hilo hadi hapa lilipofikia. Tunajua Bunge limetoa maazimio nane kwa Serikali.
Maazimio ambayo kwa sehemu kubwa Serikali ya Rais Jakaya Kikwete inatakiwa kuamua kwa kuchukua hatua dhidi ya wanaohusishwa na uchotaji fedha wa Escrow.
Ndio maana aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali Jaji Frederick Werema ameamua kuachia ngazi.
Uamuzi huo unatokana na ukweli kwamba ushauri wake kisheria hakueleweka. Jaji Werema anasema amechafua hali ya hewa.
Pia tunafahamu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Eliakim Maswi naye amsimamishwa kazi ili kupisha uchunguzi. Kisa sakata hilo hilo la Escrow.
Nani ambaye hafamu kama aliyekuwa Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi Profesa Anna Tibaijuka naye ametemwa kwenye baraza la mawaziri.
Kilichomuondoa ni kupokea fedha za Escrow.Prof. Tibajuka aliwekewa kwenya akaunti yake binafsi sh. bilioni 1.6.
Wakati mjadala huo unaendelea, hakuna mwanasiasa ambaye ameweza kupata ujasiri wa kuliambia taifa fedha hizo ni za umma au si za umma. Nani mwenye fedha hizo?.
Ujasiri ambao wanasiasa wetu walio wengi wanao hadi sasa ni kwamba sh. bilioni 306 za Escrow ni za umma. Wamesema hivyo wakiwa bungeni na wanaendelea kusema hivyo nje ya Bunge.
Kwangu mimi na hata kwa Watanzania wengine, nimefurahishwa na hotuba ya Rais Kikwete.Hotuba ambayo aliitoa Desemba 22 mwaka huu. Alikuwa anazungumza na wazee wa mkoa wa Dar es Salaam.
Kama kiongozi wa nchi ameonesha kulifahamu vema suala hilo. Akatumia nafasi hiyo kuelezea historia nzima ya sakata la Escrow.
Akaeleza namna ambavyo Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) na IPTL walivyokuwa wanalipa.
Pia, akaeleza namna ambavyo akaunti ya Tegeta Escrow iliovyofunguliwa hadi hatua ya IPTL na wanahisa wenzake kuuziana hisa na kisha kufunga akaunti ya Tegeta Escrow na kuchukua fedha zilizomo.
Rais Kikwete baada ya kutoa maelezo mengi ya kueleweka pengine kuliko yale yaliyokuwa yanatolewa na wanasiasa walio wengi akatumia nafasi hiyo kuwahakikishia Watanzania kuwa fedha hizo ni za IPTL.
Rais Kikwete katika hotuba yake alisema”Fedha hizo ni za IPTL maana ni malipo ambayo yalikuwa yanalipwa kutoka Tanesco ambazo ni tozo la uwekezaji, lakini toafuti yake fedha zilikuwa zinawekwa kwenye akaunti maalumu”.
Kimsingi hotuba ya rais imejibu swali la msingi ambalo Watanzania wengi walikosa kulisikia.Pamoja na kusema fedha hizo ni za IPTL bado akauthibitisha umma kuna kodi ya Serikali ndani yake.
Hivyo tunapoumaliza mwaka 2014, naamini rais amesema kile ambacho wengi tulipaswa kukisikia.Akasisitiza uchunguzi ufanyike na kisha sheria ichukue mkondo wake.
Akaagiza mamlaka zinazohusika na uchunguzi zitakapokamlisha taarifa , yeye atakuwa na uamuzi wa kufanya.
Baada ya kulifafanua kwa kina suala hilo, rais akatumia nafasi hiyo kuweka wazi Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo amemuweka kiporo.
Bwana we! kauli hiyo ya Prof.Muhongo kuwekwa kiporo imeamsha hasira za wanasiasa hasa za wapinzani.
Wametoa matamko ya kumtaka Rais Kikwete kumuwajibisha Prof.Muhongo kwa kumuondoa kwenye nafasi hiyo.
Wengine wametangaza kufanya maandamano nchi nzima.Najiuliza sababu za  msingi za kufanya maandamano hayo.
Najiuliza hivi wanaotaka Prof.Muhongo aondolewe kwenye nafasi hiyo ni kweli wanashinikiza kwa maslahi ya Taifa au kwa maslahi binafsi.
Hapa kuna siri kubwa, ambayo wenye kumshinikiza rais amuondoe Prof.Muhongo kwenye nafasi ya uwaziri wanaijua. Nani ambaye hajui kazi ambayo imefanywa na Prof.Muhongo kwenye wizara hiyo.
Amefanya mambo makubwa kwa maslahi ya nchi.Waziri Muhongo kwa usimamizi wake mzuri umeme umekwenda kwenye vijiji mbalimbali vya nchi yetu.
Nimezunguka wilaya za nchi hii 129 hadi sasa.Naiona kazi ambayo Prof.Muhongo ameifanya katika nishati ya umeme.
Nani ambaye hajui umuhimu wa nishati ya umeme kwa wananchi. Misimamo yake katika wizara hiyo imefanikisha ujenzi wa bomba la gesi.Angekuwa Waziri legelege , bomba la gesi kutoka Mtwara kuja(kwenda) Dar es Salaam lisingejengwa.
Alijua anasimamia maslahi ya taifa.Pia najua kwenye eneo la gesi amekasirisha wengi.Wapo ambao hawataki hata kumsikia.Leo si wakati wake kuzungumzia hilo.
Wanasiasa wanataka rais amuondoe Prof.Muhongo, hivi waziri mwingine ambaye atakwenda kwenye wizara hiyo na kukaa kwa miezi nane iliyobaki ya utawala wa rais Kikwete anakwenda kufanya jambo gani kubwa.
Kuna dhambi gani Waziri Muhongo akiachwa amalizie muda ambao Rais Kikwete ameubakisha.
Kwa kuwa tunaingia mwaka 2015, ni bora niseme ukweli maana utaniweka huru.Naamini sioni sababu ya kumuondoa Waziri Muhongo Wizara ya Nishati na Madini.
Tangu amekuwa Waziri wa Nishati na Madini Waziri Muhongo amefanya kazi kubwa na nzuri.Hata hao ambao leo wanamuandama wanajua.
Nikiri najua, haya ninayoeleza kuna watu nawakera lakini ni bora niwe huru kwenye kile ninachoamini.
Kauli ya Mwishehe, kaushauri Rais wangu, Rais Jakaya Kikwete , nakuomba umuache Waziri Muhongo amalizie kazi anayoifanya kwenye wizara hiyo.Binafsi sioni mahali ambapo Waziri Muhongo amechukua fedha za Escrow.
Sioni mahali ambapo Waziri Muhongo ameshauri fedha zitoke. Waziri Muhongo msimamo wake unajulikana wazi kuhusu fedha hizo.
Kwa bahati mbaya wanasiasa wetu wameng’ang’ania tu kumtaka rais amuondoe Muhongo badala ya kutoa suluhu ya nini kifanyike ili hayo ambayo yanatokea na kusababisha taifa kushindwa kuchukua kodi yake yasijirudie.
Wanasiasa wanashindana kuita vyombo vya habari kumshinikiza rais kumuondoa Waziri Muhongo.
Naamini na ndio ukweli wanafanya hivyo si kwasababu ya maslahi ya taifa , bali wanafanya hivyo kwa msuko mwingine. Ipo siku nitausema.Kwenye hili nitasimamia ukweli.
Kwenye siasa za Tanzania kuna mambo huwa yanakera sana. Moja ya mambo yanayokera ni pale mtu anaposimama kujifanya anapigania maslahi ya taifa kumbe, kichwani kwake anawaza tofauti.
Kuna wakati huwa najiuliza kwanini , wanashinikiza Prof. Muhongo aondolewe. Nawaza weee , lakini napata majibu tofauti tofauti. Moja ya jibu ambalo huwa nalipata ni kwamba wanaogombea urais nao wana yao kwenye hilo.
Tena si wa CCM tu, bali hata wa upinzani. Wanaona sakata la Escrow ni karata ya mwisho ya kufanikisha malengo yao.
Wengine wanaamini kupitia sakata hilo itakuwa njia rahisi ya kuiangusha Serikali ya Rais Kikwete bungeni.
Hivyo, kila mmoja analiangalia kivyake na si kweli wote wanaopigania hilo ni kwa ajili ya maslahi ya taifa. Ingekuwa ni maslahi ya taifa wangetuambia kwenye sh. bilioni 306 za Escrow za umma ziko sh. ngapi?
Nimalizie kwa kueleza tunaingia mwaka 2015, tudumishe upendo, umoja na mshikamano wetu. Najua wapo ambao watakaosema nimetumwa. Sijatumwa. Sitajali.
Kubwa zaidi kila Mtanzania ana haki ya kutoa maoni yake kwa kile anachokiamini anaweza kuchangia alau kidogo hasa kwa kuzingatia mwaka 2014 umebakisha saa chache tu wa uhai wake.
Karibu mwaka 2015, nitumie nafasi hii kuwataka mafanikio mema kwenye mwaka wa uchaguzi wanasiasa wote. Mwaka ambao kila anayetaka kugombea udiwani, ubunge au urais anarudi kuomba kura kwetu.
Nawaheshimu wanasiasa wote na wa vyama vyote. Kwenye ukweli nipo pamoja nanyi na kwenye uongo nitakuwa kando yenu.
Tuwasiliane 0767054885.

Mratibu wa Bima ya Elimu ya Bayport Tanzania, Ruth Bura kulia, akizungumza jambo katika makabidhiano ya hundi kwa bwana  Kennedy Kaupenda kushoto kwake, Makao Makuu ya Bayport, mapema wiki hii. Picha zote na Mpigapicha Wetu.
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx
TAASISI ya kifedha ya inayojihusisha na mambo ya mikopo ya Bayport Tanzania, imempatia Sh Milioni tatu mwanafunzi wa mwaka wa kwanza wa Chuo Kikuu kishiriki cha Mkwawa (MUCE), Kennedy Kaupenda, kufuatia huduma mpya ya Bima ya Elimu inayoendeshwa na taasisi hiyo nchini.

Huduma hiyo mpya ya Bima ya Elimu ya Bayport Tanzania ilianza mapema mwaka huu kwa ajili ya kuwapatia fursa wanafunzi kuendelea na masomo baada ya mzazi aliyejiunga na huduma hiyo kufariki Dunia.

Mwanafunzi wa MUCE, Kennedy Kaupenda kushoto, akizungumza baada ya kukabidhiwa hundi yake ya Sh Milioni 3 kutoka kwenye Bima ya Elimu inayoendeshwa na Bayport. Kulia kwake ni Mratibu wa Bima hiyo, Ruth Bura.   
 
Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Mratibu wa Bima ya Elimu inayotolewa na Bayport Tanzania, Ruth Bura, alisema Kaupenda alitajwa kama mnufaika kwa mzazi wake aliyefariki Dunia, hivyo waliamua kumtafuta kwa ajili ya kumpatia mafao yake kwa ajili ya kuendelea kupata elimu bila vipingamizi vyovyote.
 
Alisema huduma hiyo ina vipengele vine ambavyo ni Bronze, Gold, Silver na Exucutive, huku akisema kuwa makato ya kila mwezi ya Bronze ni Sh 2,500, ambapo fao lake ni Sh Milioni 3, wakati makato ya Gold ni Sh 6,250, huku fao lake likiwa ni Sh 7,500,000.
 
Ruth Bura, Mratibu wa Bima ya Elimu Bayport Tanzania kulia akimkabidhi hundi bwana Kennedy Kaupenda kwa ajili ya kuendelea na masomo ya elimu ya juu baada ya kufariki mzazi wake.
Mratibu wa Bima ya Elimu ya Bayport Tanzania, Ruth Bura, kulia akizungumza jambo baada ya kumkabidhi Kaupenda hundi ya Sh Milioni 3 kutoka kwenye huduma hiyo mpya iliyoanzishwa kwa ajili ya kukamilisha ndoto za elimu kwa uwapendao.
 
“Pia tunacho kipengele cha Silver ambapo makato yake kwa mwezi ni Sh 3,800, huku mteja akilipwa fao la Sh Milioni 4,500,000 na kipengele cha Executive kikihusisha makato ya Sh 9,000 na kumpatia mteja fao la Sh 10,800,000, huku tukiamini kuwa huduma hii ni sehemu ya kuhakikisha kuwa Watanzania wanawawekea ulinzi wa elimu watoto wao na yoyote wanayemchagua wao,” alisema Ruth.
 
Akizungumzia fao hilo, Kaupenda alisema hakuwa na imani kuwa angesoma vizuri baada ya baba yake kufariki, ila baada ya kutafutwa na Bayport na kutaarifiwa juu ya mafao hayo, amepata nguvu mpya.
Kennedy Kaupenda akitafakari baada ya kuiona hundi iliyoandaliwa kwa ajili yake kutoka Bayport Tanzania juu ya fao la Bima ya Elimu.
 
“Nasikitika sana baba kwa kunificha juu ya kujiunga na huduma hii sambamba na kuwa mkopaji wa Bayport, hata hivyo namshukuru kwasababu fedha hizi zimekuja kunipa mwanga mpya wa kuhakikisha kuwa nasoma kwa bidii, nikiamini kiasi cha Sh Milioni tatu kitaniweka katika wakati mzuri mno,” alisema Kaupenda, huku akiwasisitiza wazazi kujiunga kwenye huduma hiyo kwa manufaa ya familia zao.
Mbali na huduma hiyo ya Bima ya Elimu kwa uwapendao, pia Bayport inajihusisha na mikopo kwa watumishi wa umma na kampuni zilizoidhinishwa, ambapo mwishoni mwa mwaka 2014 walizindua huduma ya Mikopo ya Bidhaa, ambapo bidhaa za bodaboda aina ya Lifan, Toyo na Boxer zinakopeshwa kwa wateja wa Bayport Tanzania.

unnamed 
Mahabusu ambaye jina lake halikupatikana mara moja akiwa amenasa kwenye ukuta wa chuma baada ya kupigwa risasi na maaskari wakati alipokuwa akijaribu kutoroka kwa kuruka ukuta huo katika mahakama ya Kisutu jijini Dar es salaam, inadaiwa  mahabusu huyo ambaye si raia wa Tanzania alikuwa anakabiliwa na kesi ya madawa ya kulevya.
unnamed2
Baadhi ya askari na watu mbalimbali wakiangalia tukio hilo lililotokea leo asubuhi katika mahakama ya kisutu
unnamed1
Maaskari wakimtoa kwenye ukuta huo wa chuma
V.S

MOTO mkubwa umeteketeza maduka 18 katika mtaa wa Kwakivesa wilaya ya Handeni mkoani Tanga baada ya lori lililokuwa limebeba mafuta kugonga nguzo ya umeme kupinduka na kisha kuanza kuwaka moto uliosambaa hadi kwenye maduka hayo.
Taharuki hiyo imetokea leo majira ya saa 5:00 asubuhi baada ya lori hilo lililokuwa kwenye mwendo kasi kutaka kumkwepa mwendesha bodaboda na kujikuta likiacha njia na kugonga nguzo ya umeme na kusababisha hasara kubwa kwa wananchi huo.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tanga, Frasser Kashai amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kudai kuwa moto huo ulitokea saa 5.asubuhi katika mtaa huo kufuatia roli la mafuta aina ya Fuso kugonga nguzo ya umeme na kusababisha betri kutoa cheche zilizosababisha moto kuanza kuwaka.
Kamanda Kashai amesema roli hilo lilikuwa likiendeshwa na dereva Ali Makelele ambaye bado hajapatikana huku utingo wake aliyemtaja kwa jina moja la Mfundo akiwa amekimbizwa hospitali ya Wilaya ya Handeni kwa matibabu Zaidi baada ya kuungua vibaya.
"Moto ulianza kuliteketeza roli hilo la mafuta na baadaye ukasambaa kwenye maduka jirani ,hali ilikuwa mbaya sana, hadi sasa hatujajua hasara iliyopatikana, tutakapokuwa na taarifa kamili tutawataarifu", amesema kamanda Kashai.
Aidha mashuhuda wa tukio hilo wanaeleza kuwa moto huo ulishika kasi kwa haraka kutokana na hali ya hewa kuwa ya upepo mkali licha ya juhudi za wananchi kuuzima lakini uliwashinda nguvu.
Aidha jeshi la polisi limelaani mtindo unaoota mizizi hivi sasa wa wananchi kujichukulia sheria mkononi kwani baada ya tukio la moto kutokea kikosi cha zimamoto kutokea Korogwe kilifika katika eneo la tukio lakini badala ya kuachwa kufanya kazi yake kikashambuliwa.
Shambulio hilo la wananchi kwa zimamoto limesababisha hasara ikiwa ni pamoja na kuvunjwa vioo vya gari, kupotea kwa vitendea kazi pamoja na baadhi ya askari wa zimamoto kujeruhiwa.
CHANZO:MWANANCHI


















Monday 22 December 2014


1q
Rais Dr Jakaya Kikwete amemuachisha kazi waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo  Makazi Profesa Anna Tibaijuka kutokana na tuhuma za kupata mgao wa Fedha za Akaunti ya Escrow kiasi cha bilioni Moja na Milioni Mia Sita ambazo alidai amepewa mchango kwa ajili ya shule, Rais Jakaya amesema Tumeamua mwenzetu huyu atupishe ili tuchague mtu mwingine wa kuhudumu katika wizara hiyo kutokana na maswali magumu.
Akiwa kama Mtumishi wa serikali ambaye anatakiwa kufuata maadili ya Utumishi  wa umma  aliamua kupokea kiasi kikubwa cha fedha huku akijua kimaadili kama mtumishi wa serikali haitakiwi, Rais Dr. Jakaya Kikwete amesema hayo wakati  akizungumza na taifa kupitia Wazee wa Dar es Salaam leo katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.
Kwa upande wa Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo na Katibu Mkuu wa Wiazara hiyo Eliackhim  Maswi  amesema ameagiza uchunguzi ufanyika na katika muda wa siku mbili au tatu hivi atapewa taarifa ya uchunguzi huo na kuchukua hatua stahiki.
Na Kwa upande wa Majaji wa Mahakama Kuu waliotuhumiwa Rais Dr. Jakaya Kikwete amesema anamwachia Jaji Mkuu Mh. Jaji Mohammed Chande Othman ili achukue hatua za kimaadili kutokana na taratibu za kimahamama na mara baada ya kujiridhisha atapewa taarifa na Jaji mkuu na kuchukua hatua.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Jakaya Kikwete   
Rais Jakaya Kikwete ametengua nafasi ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka kupitia hotuba aliyotoa kuzungumzia kashfa ya upotevu wa fedha kutoka akaunti ya Tegeta Escrow.
Hatua hiyo imechukuliwa na Rais Kikwete mbele ya wazee wa Dar Es Salaam aliokuwa akiongea nao na matangazo kurushwa moja kwa moja kupitia televisheni ya taifa na vyombo vingine.
Uchunguzi uliofanywa na kamati ya hesabu za umma ya Tanzania (PAC), ilidai kuwa Profesa Tibaijuka ni mmoja wa watu walionufaika kinyume cha sheria kwa kupata fedha zilizotoka katika akauti hiyo iliyofunguliwa kutunza fedha kusubiri ufumbuzi wa mgogoro wa kibiashara kati ya kampuni ya kusambaza umeme TANESCO na kampuni binafsi ya kuzalisha umeme ya IPTL.
Siku chache zilizopita Profesa Tibaijuja aliitisha mkutano na waandishi wa habari jijini Dar Es Salaam kubainisha kuwa hakuwa akikusudia kujiuzulu kutokana na tuhuma zilizokuwa zikimkabili.
Hata hivyo Rais Kikwete hakutangaza kuwachukulia hatua watumishi wengine waliodaiwa kuhusika na tuhuma hiyo kwa maelezo kuwa uchunguzi zaidi unatakiwa kwa kila mtuhumiwa.
Kumekuwa na ubishi mkubwa kujadili endapo fedha ambazo ni mabilioni zilizochukuliwa zilikuwa za umma au la. Na hata Rais Kikwete amesema maelezo aliyopewa na wataalam yanaonyesha hazikuwa mali ya TANESCO.
                                             V.S
Masikio ya Watanzania leo yameelekezwa kwa Rais Jakaya Kikwete watakapokuwa wakisikiliza hotuba yake kwa Taifa inayotarajiwa kujibu maswali yapatayo 10 ambayo yanatarajiwa kutegua kitendawili cha kashfa ya uchotaji wa Sh306 bilioni katika Akaunti ya Tegeta Escrow.
Maswali hayo yanatokana na maazimio ya Bunge ambayo yalionekana kuvuta hisia za wananchi katika kona mbalimbali za nchi ambako walikuwa wanafuatilia moja kwa moja mjadala wa Bunge hadi kupitishwa maazimio hayo.
Hotuba hiyo inayotarajiwa kutolewa wakati Rais atakapozungumza na wazee wa Dar es Salaam, ikiwa ni siku nne baada ya Kampuni za IPTL na Pan Africa Power Solutions (PAP) kukimbilia mahakamani kuzuia utekelezwaji wa maazimio ya Bunge.
Baadhi ya wasomi nchini wamesema hatua ya kuzuia utekelezaji wa maazimio hayo pamoja na kauli ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka kuwa akijiuzulu Rais atamshangaa, ni mambo yanayofanya hotuba ya Rais kusubiriwa kwa hamu.
Swali la kwanza ambalo wananchi wanasubiri jibu lake ni iwapo Rais Kikwete atatuliza kiu yao kuhusu kashfa hiyo ambayo imekuwa gumzo nchi nzima na hivyo kulegeza msimamo wa wahisani wa kuinyima nchi misaada.
Pili, wananchi wanasubiri kusikia iwapo Rais Kikwete ataagiza uchunguzi zaidi wa Takukuru, Polisi na vyombo vingine kama ambavyo azimio la kwanza la Bunge linavyotaka wahusika wachukuliwe hatua za kisheria kuhusika na vitendo vyote vya kijinai kuhusiana na miamala ya Akaunti ya Tegeta Escrow.(MM)
Tatu, wanasubiri kwa hamu kuona hatua ambayo Rais Kikwete atachukua dhidi ya Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Eliakim Maswi pamoja na Profesa Tibaijuka kutokana na kutajwa katika maazimio hayo ya Bunge.
Kwa nyakati tofauti, viongozi hao wamekaririwa wakisema kuwa hawahusiki na kashfa hiyo. Mbali ya Profesa Tibaijuka kujitokeza kujitetea mwenyewe, baadhi ya wananchi wamejitokeza kuwatetea na kuwasafisha viongozi hao katika vyombo vya habari na mitandao ya kijamii.
Nne, Je, atatengua uteuzi wa Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Umeme (Tanesco) ambayo pia ilitakiwa kuwajibishwa ikiwa chini ya Mkuu wa Majeshi mstaafu, Jenerali Robert Mboma.
Tano, ili kuwachukulia hatua majaji waliotajwa, Aloysius Mujulizi na Profesa Eudes Ruhangisa, Rais Kikwete anatakiwa aunde Tume ya Kijaji ya kuchunguza tuhuma za utovu wa maadili zinazowakabili, kinachosubiriwa kwa hamu ni kuona endapo ataunda tume hiyo.
Swali la sita linalohitaji jibu linahusu kupambana na kudhibiti vitendo vya rushwa kubwa, ufisadi na hujuma za uchumi. Kinachosubiriwa ni jibu la Rais Kikwete iwapo Serikali itaandaa na kuwasilisha muswada wa marekebisho ya sheria iliyoiunda Takukuru kwa lengo la kuanzisha taasisi mahsusi itakayoshughulikia masuala hayo.
Vilevile, wananchi wanatazamia kupata suluhisho la gharama kubwa za umeme katika jibu la Rais Kikwete iwapo Serikali iko tayari kuinunua mitambo ya Kampuni ya IPTL kama ilivyopendekezwa na Bunge kwa lengo la kuokoa fedha za Tanesco zinazotumika kununua umeme kwa bei ya juu.
WANANCHI

Friday 19 December 2014

MKUU wa Polisi Wilaya ya Mjini, Ali Makame (wa pili kushoto) akiangalia gari iliyovunjwa na kuibiwa pesa zinazosadikiwa kuwa ni euro elfu moja na shilingi za kitanzania milioni tano, muda mfupi baada ya kufika eneo la tukio katika eneo la Mlandege mjini Zanzibar.
ASKARI Polisi wakiwa wameizunguka gari iliyovunjwa na kuibiwa pesa zinazosadikiwa kuwa ni euro elfu moja na shilingi za kitanzania milioni tano, tukio hilo limetokea majira ya saa saba mchana katika eneo la Mlandege mjini Zanzibar leo. Mmiliki wa gari hiyo aliegesha gari yake na kuingia msikitini kwa kusali sala ya Ijumaa katika msikiti jirani na maengesho ya gari katika eneo la mlandege. (Picha na Haroub Hussein).


Kwa nchi nyingi za Afrika hasa Tanzania zinapiga marufuku kubwa ya uonyeshwaji wa movie za ngono kutokana na kwamba hazina maadili mazuri kwenye jamii, ukienda nchi kama China wao wameenda mbali zaidi, sheria kali zimewekwa ili kuzuia kabisa mtu yeyote kucheza filamu hizo, ama kuuza.

Nchi za Ulaya na Marekani zimekuwa zikishutumiwa kuruhusu biashara zote, kutengeneza na kuuza movie hizo, lakini hii kutoka Los Angeles, Marekani imeweka sheria inayowalazimu waigizaji wa filamu hizo za ngono kuvaa mipira maalum ya kuwakinga na maambukizi ya magonjwa, Condom.

Sheria hii ambayo iliyoanza kama muswada mwaka 2012 inawalazimu waandaaji wa filamu hizi pia kulipia ada maalum ili kupewa kibali cha kufanyia kazi hiyo.

Waandaaji wengi wa filamu za ngono wamelalamikia sheria hii wakidai kuwa inakwenda kinyume na haki zao za msingi japo Mahakama imetoa tayari msimamo wake.

Wadau wa industry ya filamu hizo wamedai kuwa wanafahamu fika hatari zilizoko kwenye maambukizi na wanachukua hatua za kupunguza maambukizi haya kwa kuwakinga na kuwapima watu wote wanaoshiriki uigizaji wa filamu hizi kabla ya kuingia nao mikataba ambapo utaratibu huu mpya unawapa hofu waandaaji hao kwamba huenda soko la biashara yao likayumba

Mto wa kuchegama watumika kuondoa uhai wa watoto wadogo ndugu wawili. 
Mtanzania aishiye Melbourne,Australia,Charles Mihayo mwenye umri wa miaka 36,aliyekuwa akituhumiwa kwa mauaji ya binti zake wawili,amehukumiwa kifungo cha maisha jela.
Mihayo ametiwa hatiani baada ya mahakama kujiridhisha kwa ushahidi uliothibitisha kwamba aliwaua binti zake ,,Indiana aliyekuwa na umri wa miaka mitatu na Savannah aliyekuwa na umri wa miaka minne kwa kuwaua kwa kuwabana kwa mito ya kulalia na hivyo kukosa hewa.
Waendesha mashtaka walisema kwamba, Mihayo alitenda kosa hilo baada ya kuingia kwenye mgogoro mzito na mama wa watoto aliyewahi kuwa mkewe kwa minajili ya kujilipiza kisasi.
Akitoa hukumu hiyo jaji wa mahakama kuu ya Victorian,Lex Lasry alisema ugomvi na mkewe haikuwa sababu ya kujiaminisha kutenda kosa la mauaji na kushangazwa na namna mtuhumiwa alivyotumia nafasi ya ugomvi na mkewe wa zamani kuwaua watoto ili kupunguza machungu yake.
Inaelezwa kuwa Mihayo alituma ujumbe mfupi wa maneno kwa mtalaka wake kumfahamisha kuwa ameshinda na anakubali kupoteza haki yake ya kuwaona watoto hao, kisha akawapiga picha watoto hao wakicheza muziki muda mfupi kabla na kuwaweka pamoja na kuwabana pumzi kwa kutumia mito ya kulalia,kisha kupiga simu polisi na walipowasili eneo la tukio, aliwaambia "nimekamilisha,nimewaua watoto wInaelezwa kuwa Mihayo alituma ujumbe mfupi wa maneno kwa mtalaka wake kumfahamisha kuwa ameshinda na anakubali kupoteza haki yake ya kuwaona watoto hao, kisha akawapiga picha watoto hao wakicheza muziki muda mfupi kabla na kuwaweka pamoja na kuwabana pumzi kwa kutumia mito ya kulalia,kisha kupiga simu polisi na walipowasili eneo la tukio, aliwaambia "nimekamilisha,nimewaua watoto wangu"
                                                  V.S

Rais Jakaya Kikwete 
Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete leo atalihutubia taifa la nchi hiyo ambapo anatarajiwa kuyatolea ufafanuzi masuala nyeti yanayoligusa taifa hilo.
Wadadisi wa masuala ya kisiasa na kijamii wanatabiri huenda hatua atakazozichukua dhidi mawaziri na maafisa wa serikali waliohusika na ufisadi wa mamilioni ya fedha katika akaunti ya Escrow itakuwa ni moja kati ya agenda muhimu atakayoitolea ufafanuzi.
Hotuba hiyo inakuja wakati kukiwa na shinikizo kutoka kwa baadhi ya raia na wapinzani wakitaka hatua zaidi zichukuliwe kutekeleza azimio la bunge ambalo linatataka mawaziri na maafisa wa serikali waliohusika na sakata hilo la ufisadi wawajibishwe ikiwa ni pamoja na kufukuzwa kazi.
Watu wakubwa serikalini akiwemo waziri mkuu Mizengo Pinda walihusishwa na Kashfa ya Ecrow na kutakiwa kujiuzulu 
 
Sakata la Akaunti ya Escrow liliibuliwa bungeni na mmoja wa wabunge wa bunge la Tanzania, David Kafulila na kusababisha mjadala mkali na kuamua Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kupewa jukumu la kuchunguza kashfa hiyo.
Baada ya uchunguzi kuwasilishwa katika mkutano wa bunge uliomalizika mwishoni mwa mwezi Novemba, kamati hiyo ilikuja na maazimio manane kuhusu taarifa ya ukaguzi maalum kuhusiana na miamala iliyofanyika katika akaunti ya Escrow ya Tegeta pamoja na umiliki wa kampuni ya IPTL.
Miongoni mwa maazimio ya bunge yaliwataja baadhi ya wanasiasa, mwanasheria mkuu, maafisa waandamizi wa serikali, majaji, wakuu wa taasisi za umma, viongozi wa dini, mawakili wa kujitegemea na watu binafsi kuhusika katika kashfa hii na hivyo kuagiza mamlaka zinazohusika kuwachukulia hatua za kisheria wahusika na wengine kuondolewa katika nyadhifa zao za kuteuliwa,tayari Mwanasheria mkuu wa serikali amekwisha jiuzulu na rais kukubali uamuzi huo.
Akaunti ya Escrow ilianzishwa katika Benki Kuu ya Tanzania ili kuhifadhi fedha, baada ya kuibuka kwa mvutano kati ya Shirika la Umeme la Tanzania, Tanesco na kampuni ya kufua umeme ya IPTL kuhusu ongezeko la mtaji wa uwekezaji, huku TANESCO ikilalamika kuwa gharama za kununua umeme kutoka kampuni ya IPTL zilikuwa za juu mno. Fedha hizo zingeendelea kutunzwa katika Akaunti hayo hadi wakati ambapo suluhisho la mvutano wa wabia hao wawili lingepatikana.
                                                    V.S
mkuu wa wilaya ya songea akifungua mkutano kati ya wataalam wa misitu na wafanyabiashara wa mazao ya misitu wilaya ya songea mkaoni Ruvuma.
Mkuu wa wilaya ya songea akitoa msisitizo wa kusimamia sheria za uvunaji wa misitu ili kuepuka kutokea kwa jangwa katika maeneo ya wilaya ya songea.


meneja wa wakala wa huduma za misitu wilaya ya songea bi Manyisye Kibona Mpokigwa  pamoja na kaimu mkurugenzi halmashauri ya wilaya ya songea bwana godifrei chipakapaka.
Baadhi ya mabwana miti wilaya ya songea wakifuatlia kwa umakini mkubwa katika mkutano huo uliofanyika katika ukumbi wa maliasili wa mkoa wa Ruvuma.

wafanyabiashara wachache wakisiliza mada ya mabadiliko ya taratibu za uvunaji na biashara ya mazao ya misitu.

MAELEZO NA MATHIAS PONDAMALI.
imeelzwa kuwa utaratibu wa uvunaji wa miti kwa ajili ya mkaa,mbao na kuni ni pamoja na uvunaji huo ufanyike katika eneeo lililoruhusiwa tu,uvunaji kwa ajili ya mbao hauruhusiwi kuanusha mti kabla ya kupima kipenyo,haiuhusiwi kuchana magogo kwa kutumia msumeno wa mnyororo(chainsaw.

Lakini pia utaratibu wa usafirishaji wa mazao ya misitu kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine
>kabla ya kuanza kusafirisha mazao ya misitu hakikisha umelipa ushuru wa serikali kuu na wa halmashauri ya wilaya.
>kila mfanyabiashara wa mazao ya misitu lazimaawe bna hati ya kusafirisha anapotoka sehemu moja kwenda nyingine
>Hairuhusiwi kusafirishaji mazao ya misitu yakiwemo mazao ya mkaa na kuni zaidi ya saa kumi na mbuili jioni na kabla ya saa kumi na mbili asubuhi.
>Mazao yote ya misitu kama vile mbao,mkaa,samani au kuni yatakayoyatakayosafirishwa kwa njia ya yoyote kama vile magari madogo pikipiki baiskeli,mikokoteni,baiskeli na nk.
>nyaraka zinazohusika zikaguliwe.

Thursday 18 December 2014

















                                                                                                               V.S